Mkurugenzi wa Mji Newala anawatangazia watu wote kwamba Mradi wa upimaji wa viwanja katika eneo la Amkeni - Luchingu umekamilika. Wananchi wote wanakaribishwa kuja kununua viwanja hivyo kwa ajili ya Makazi na Biashara, Biashara na Makazi. Bei ya fomu za maombi ni shilingi 20,000 na bei kwa square mita ni shilingi 2,200 kwa viwanja vya makazi, shilingi 2,300 kwa viwanja vya biashara na shilingi 2,500 kwa viwanja vya makazi na biashara. Jumla ya viwanja vipo 433. Nyote Mnakaribishwa.
Newala-Mtwara
Anwani ya Posta: P.O.BOX 39
Simu: (+255) 023 2935398
Mobile: PS (0684439199)
Barua pepe: info@newalatc.go.tz
Haki milikiĀ©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa