• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Byakanwa aipa tano Halmashauri kwa kupata hati safi kutoka ofisi ya CAG

Posted on: June 3rd, 2020

Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imeipongeza na kuipatia hati safi halmashauri ya mji Newala kwa usimamizi nzuri wa fedha za serikali na kutekeleza kikamilifu miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Pongezi hizo zimetolewa leo Jumatano Juni 03, 2020 mbele ya mkuu wa mkoa wa Mtwara na Bi. Mary Wembe, Ofisa kutoka Ofisi ya CAG makao makuu katika kikao cha baraza la hoja cha halmashauri hiyo, ambapo katika taarifa yao imeonyesha hoja 18 zilizojitikeza 10 zimeshapatiwa majibu na 8 zilizosalia zinaendelea kupatiwa ufumbuzi.

Mara baada ya kupokea taarifa hiyo Mkuu wa mkoa Mtwara Gelasius Byakanwa, amempongeza Mkuu wa wilaya, mkurugenzi, watumishi, mwenyekiti wa halmashauri pamoja na madiwani kwa kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi kikamilifu na kusimamia fedha za umma kwa uaminifu pasipo kujali maslahi yao binafsi na itikadi za vyama.

Aidha amesema mafanikio hayo yanaonyesha wazi kuwa kuna mshikamano wa kiutendaji baina ya ofisi ya mkuu wa wilaya, ofisi ya mkurugenzi pamoja na madiwani kwani hata hoja zilizojitokeza zingine haziusiani na halmashauri na zile za halmashauri zimeshaanza kupatiwa majibu, hiyo inaonesha umakini wa kiutendaji.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Newala Bi. Aziza Mangosongo amesema halamashauri hiyo ni mfano wa kuigwa, kwa kuwa imetekeleza baadhi ya miradi kwa fedha zake za ndani zikiwapo zahanati 4, miradi mingine ni matundu 240 ya vyoo kupitia kapeni ya mkuu wa mkoa ya shule ni choo, madarasa 49 kwa shule za msingi na 30 kwa shule sekondari, mabwalo matatu (3) pamoja na maabara tatu (3).

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Andrew Mgaya amesema katika mapendekezo 18 ya hoja za CAG mapendezo saba tayari zimeshafanyiwa kazi na kufungwa, mapendekezo matatu yamehamishiwa RUWASA na mapendezo mengine nane yapo kwenye hatua za utekelezaji ili kumaliza hoja hizo.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Sambili Mohamedi amebainisha kuwa mafanikio hayo, yametokana mtazamo wa kupeleka maendeleo kwa wananchi na kuachana na itikadi za kisisasa ukizingatia halamshauri hiyo ilikuwa na madiwani wa vyama tofauti vya kisiasa na kuwataka hata wale watakao endelea baadae kuendeleza na ushirikiano huo.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa