• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri imetumia shilingi milioni 120 za mapato yake ya ndani kuanzisha sekondari

Posted on: July 17th, 2023

Halmashauri ya Mji Newala imetumia shilingi milioni 120 za mapato yake ya ndani, kuanzisha shule mpya ya sekondari katika ukanda wa mto Ruvuma inayotarajia kuanza mwezi Januari mwaka 2023.

Akizungumzia ujenzi wa sekondari hiyo Jumatatu 17 Julai, 2023, Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini Mhe. George Mkuchika amesema halmashauri imechukua hatua hiyo kutokana na kuona adha wanaoipata wanafunzi wanaotoka ukanda huo ambao wanatumia zaidi ya kilomita 10 kufuata masomo.

Mhe. Mkuchika akiwa anaendelea na mikutano jimboni mwake amesema, halmashauri ilishatekeleza sera ya serikali ya elimu ya kuwa na sekondari kwa kila Kata, lakini waliona upo umuhimu wa kuanziasha shule hiyo ili kutimiza ndoto ya elimu kwa watoto zinazokwamishwa na utoro unao tokana na umbali.

“Sisi madiwani tuliona adha wanayopata watoto wakati wa masika na hata umbali ulipo wanapandisha mlima huu kila siku kwenda tu ni zaidi ya kilometa 10 tukasema lazima tuwe na shule ya sekondari huku chini na matokeo yake ndio haya” Alieleza Mhe. Mkuchika

Wananchi wa kata za Nanguruwe, Mcholi 1 na Mkunya wametoa shukrani zao kwa halmashauri, na kupitia taarifa iliyosomwa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Mcholi 1 Ndg. Bwamkuu Ally, imebainisha katika awamu ya kwanza halmashauri ilitoa shilingi Milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi, nyumba ya mtumishi, pamoja na matundu sita ya vyoo.

 Aidha wameeleza kuwa ujenzi wa awamu ya kwanza umekamilika isipokuwa nyumba ya mtumishi ambayo ipo kwenye hatua ya ukamilishaji na awamu ya pili halmashauri imetoa shilingi milioni 40 kwa ajili ya vyumba viwili vya madarasa ambavyo ujenzi wake unakaribia kukamilika.

Hata hivyo akiwa katika vijiji vya Chiunjila, Chihanga na Mapili vijiji lengwa vya shule hiyo walimuomba apendekeze jina la shule ambapo alipendekeza iitwe Benjamini Mkapa Sekondari na wananchi waliridhia pendekezo hilo.

Afisa mipango wa Halmashauri ya Mji Newala Bi. Sophia Makungu amesema halmashauri itaendelea kutenga fedha za mapato ya ndani kutekeleza miradi mbalimbali itakayoibuliwa na wananchi huku akiwasisitiza kuendelea kujitolea wakati wa utekelezaji ikiwa ni sehemu ya mchango wa jamii.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa