• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya mji Newala imeanza kutekeleza agizo la kuwaondoa wanaoshikilia maeneo skimu za umwagiliaji

Posted on: September 11th, 2019

Halmashauri ya mji Newala imeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa la kuwaondoa wananchi walioshikilia maeneo bila kuyafanyia kazi katika miundombinu ya umwagiliaji ya Chikwedu Chipamanda na Lipeleng’enye.

Hayo yamebainishwa na Ofisa kilimo na umwagiliaji anayesimamia miundombinu hiyo Bw. Nelson Mtunga wakati wa kuanza zoezi la kimkakati la kusafisha mifereji na kuwatambua wanaomiliki maeneo kwenye skimu ya umwagiliaji ya Chikwedu Chipamanda lililoanza hii leo Jumatano 11/09/2019.

Bwana Mtunga amesema serikali kupitia wafadhili walishaweka miundombinu ya umwagiliaji katika skimu hizo na kutokana na changamoto ya wakulima wengi kutoyafanyia kazi maeneo yao, Mkuu wa Mkoa aliagiza mashamba yao wapewe vijana waliotayari kulima na kujiongezea kipato ili kulinda miundombinu hiyo na kufikiwa lengo kusidiwa la serikali la kuwanufaisha wananchi.

Mtunga alisema “kwa upande wetu kama halmashauri kwa kushirikia na watendaji wa vijiji tumeamua kuwatambua wamiliki kwa majina na ukubwa wa mashamba yao lakini jambo la muhimu ni hili ambalo tumelianza leo, kwanza kusafisha hii mifereji zoezi linalowahusu watu wote wenye maeneo na wasionao, tumepanga wale watakaoshindwa kushiriki tutayachukua maeneo yao na kuwamilikisha wengine kwa taratibu zote za kisheria, lakini vilevile wenye maeneo makubwa wanaoshidwa kuyamudu kuyafanyiakazi itabidi tuyapunguze na kuwapatia watu wengine”.

Katibu wa umoja wa wamwagiliaji wa skimu hiyo Bw. Juma Mnonji amesema amefurahishwa na hatua hiyo ya halmashauri, kwani bonde hilo ni muhimu kwa shughuli za uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa umjula na katiba yao inaelekeza adhabu kwa wale wasioshiriki usafi, ambayo ni kulipa faini hadi shilingi laki moja (Tsh. 100,000/=).

Hatahivyo amesisitiza kuwa ili kufikia lengo, ni lazima kuwe na ushirikiano baina ya umoja huo na serikali kupitia halmashauri, isimamie zoezi hilo kwani uzoefu unaonyesha watu hawajitumi pasipo kuongozwa na kusimamiwa hasa na viongozi wa juu, huku akifafanua kuwa umoja wa mwagiliaji na wananchi wanaozunguka bonde hilo, wamekubaliana kufanya usafi kwa pamoja kila Jumatano na Jumamosi.

Baadhi ya wakulima na wasio wakulima walioshiriki zoezi hilo, wamesema skimu hiyo ni muhimu kwa kujiongezea kipato na kujikimu na maisha yao, hivyo wanaomba wale walioyatelekeza mashamba na wenye mashamba makubwa wangepungiziwa ukubwa au kunyang’anywa na kupatiwa vijana wenye nguvu ili wayaendeleze.

Skimu ya bonge la Chikwedu Chipamanda lipo Kijiji cha Chikwedu, Kata ya Mcholi 1, Tarafa ya Mkunya halmashauri ya mji Newala Mkoani Mtwara, na ina ukubwa wa hekta 1200 lakini halitumiki hata kwa kiasi cha nusu yake.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa