• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya mji Newala imepokea vitambulisho vya wajasiriamali wadogo 1200

Posted on: May 26th, 2020

Halmashauri ya mji Newala leo Jumanne Mei 26, 2020 imepokea vitambulisho vya wajasiriamali 1200 kwa ajili ya kuanza kuwauzia wajawasiriamali wadogo huku wasimamizi wa zoezi hilo wakitakiwa kujiepusha na ubadhirifu.

Akikabidhi vitambulisho hivyo kwa Afisa biashara wa halmashauri ya mji Newala, Mkuu wa wilaya Newala Bi. Aziza Mangosongo amesema mwaka jana wilaya ya Newala ilifanya vizuri kwenye mauzo, hivyo ni wajibu wa watendaji kusimamia kikamilifu na uadilifu.

Aidha Mhe. Mangosongo  amewakata watendaji ambao wanasimamia zoezi hilo kuhakikisha wanatunza kumbukumbu zao vizuri na kuacha kujikopesha fedha za mauzo ili kujiepusha na tuhuma ubadhilifu na matumizi mabaya za fedha za umma.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndg. Andrew Mgaya, mara baada ya kupokea vitambulisho hivyo amewataka watendaji kwenda kuuza vitambulisho hivyo kwa wajasiriamali wadogo pekee kwa kuwa wafanyabiashara wengine wenye namba za utambulisho (TIN) wana utaratibu wao wa kulipa kodi ya mapato.

Hata hivyo ameeleza kuwa sasa hivi serikali imeweka utaratibu nzuri wa malipo hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha fedha zinaelekezwa mahali sahihi, zilipiwe benki kwa kutumia control namba huku akiwaonya wale watakaobainika kufanya kosa la wizi wa fedha watachukuliwa hatua za kiutumishi.

Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi Ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani Newala, Kamanda Edwin Mukama, amesema kazi ya TAKUKURU ni            kufuatilia fedha za umma na hizo fedha umma hivyo atakayebainika kufanya kosa, atakuwa ni muhujumu uchumi na kosa hilo halina dhamana na ukibainika mahakani adhabu yake ni kifungo cha miaka 25 hadi 20, hivyo kila mmoja azingatie maelekezo na kujua wajibu wake.

Akimuwakilisha Kamanda wa Polisi wilayani hapa, Mkuu wa kituo cha Polisi Newala SP. Apolinary Mwangailo amesema jeshi hilo halitakuwa huruma kwa wale watakaobainika na makosa, kwa kuwa maelekezo yote yameshatolewa na wajibu sio kuwaonea huruma wafunjifu wa sheria na taratibu.

Zoezi la ugawaji vitambulisho hivyo ni hatua ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwatambua na kuwashirikisha wajawasiriamali wadogo kuchangia maendeleo ya Taifa na mwaka huu 2020 limeigia awamu yake pili vikiwa limefanyiwa maboresho ya taarifa za mjasiriamali, makundi ya wajasiriamali wanastahili pamoja fumo wa malipo.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa