• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

HALMASHAURI YA MJI NEWALA YAANZA KUTOA MKOPO WA 10% SHILINGI MILIONI 292.8 KWA MFUMO JUMUISHI WAKISHIRIKIANA NA NMB

Posted on: September 4th, 2025

Halmashauri ya Mji Newala kwa mwaka 2024/2025 imetekeleza sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kutoa mikopo jumuishi ya asilimia 10% yenye thamani ya shilingi milioni 292.8 kwa makundi lengwa ya vijana, wanawake na makundi maalum.

Mkuu wa Wilaya ya Newala Alhaj. Mwangi Kundya, akiwa katika hafla ya kukabidhi hundi mfano kwa vikundi vya wajasiriamali, ameipongeza halmashauri hiyo kwa kutekeleza sera hiyo iliyolenga kuinua mitaji na kuwaongezea mapato wafanyabiashara wadogo.

“niwapongeze kutenga fedha na pia kuwaibua wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika kuwekeza katika shughuli mbalimbali za kibiashara ili kujipatia mapato ni Imani yangu fedha hizi zitaendelea kufanyakazi kama zilivyo kusudiwa”

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndg. Geofrey Nnauye amesema mfumo jumuishi wa utoaji mikopo 10% kwa kushirikiana na baki upo kwenye matazamio, hivyo vikundi vinapaswa kutekeleza makubaliano ili kuleta ufanisi.

“Halmashauri ya Mji Newala tuanatoa mikopo kwa kushirikiana na benki ya NMB, kwasababu tumeingia kwenye mabadiliko haya niwaombe yale mazoea ya kule nyuma ya ukusanyaji na urejeshaji wa fedha tubadilike tusije kuukwamisha mpango wa taifa”,

Naye Afisa maendeleo ya jamii wa Mkoa wa Mtwara Bi. Thabitha Kilangi ameiomba banki ya NMB pamoja na maafisa maendeleo wa halamshauri kuendelea kuwajengea uwezo wajasiriamali hao kwa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara ili wakue kiuchumi kutokana na shughuli zao.

Afisa Maendeleo ya jamii wa Mji Newala Bi. Joyce Israel ameeleza kuwa 2024/2025 kulikuwa na maombi ya mkopo kutoka kwa vikundi 115 na baada ya kamati za uhakiki vikundi 89 vilihidhinishwa kupata mkopo.

Aidha Israeli amefafanua kuwa, Vikundi 60 vimepokea fedha shilingi milioni 292.8 kwa awamu ya kwanza 33 vikiwa vya wanawake, 13 vya vijana na vikundi 9 vya watu wenye ulemavu huku vikundi 29 vilivyobaki vitapokea shilingi milioni 59.2 katika robo ya pili ya 2025/2026.

Meneja wa mauzo kanda kusini wa benki ya NMB Ndg. Frank Njawala akimwakilishi meneja wa kanda hiyo amesema kipaumbele kimojawapo cha benki yake ni kuwafikia wafanyabiashara wadogo hivyo wamejipanga kushirikiana nao mpaka wafikie hatua ya mafanikio.

Hata hivyo Njawala amefahamisha kuwalinda wafanyabiashara wadogo kwa kuwa tafiti za jukwaa la Uchumi duniani zinaonesha biashara ndogo zinachangia nusu ya pato la taifa pamoja na kuongeza ajira kwa wastani wa 80% ya ajira zote kwa nchi za afrika.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA UDEREVA September 01, 2025
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI NNAUYE AWASHUKURU JHPIEGO KWA KUSHIKISHA JAMII ELIMU YA SARATANI YA MATITI

    September 11, 2025
  • WATAHINIWA 2516 HALMASHAURI YA MJI NEWALA KUHITIMU DARASA LA SABA 2025

    September 08, 2025
  • DC KUNYA AITAKA JAMII IWAANDALIE WAZEE MAZINGIRA BORA ILI KUPUNGUZA UTEGEMEZI

    September 05, 2025
  • MKUU WA WILAYA NEWALA AWATAKA WAZEE WA MKOA WA MTWARA KUSAIDIA KUIMARISHA MAADILI YA VIJANA

    September 04, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa