• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya mji Newala yapenga matundu 240 ya vyoo, kampeni ya shule ni choo

Posted on: July 17th, 2020

Watendaji wa Serikali ngazi ya Kata na Vijiji wa halmashauri ya Mji Newala wametakiwa  kusimamia miradi ya maendeleo kwa kuishirikisha jamii ya maeneo husika kwa kuwa wao ndio wanufaika wa moja kwa moja hivyo inawapasa washiriki kwenye hatua za utekelezaji.

 Wito huo umetolewa jana Alhamisi Julai 16,2020 na Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo wakati anahitimisha ziara yake ya kukagua utekelezaji wa ujenzi wa matundu ya vyoo katika halamshauri hiyo kupitia kampeni ya shule ni choo iliyoasisiwa na Mkuu wa mkoa wa Mtwara.

Mhe. Mangosongo ameipongeza hatua iliyofikiwa na halamashauri hiyo kwa kujenga matundu 240 ya vyoo tangu kuanza kwa kampeni hiyo lakini amewakosoa baadhi ya Watendaji wa Kata na Waratibu Elimu Kata, kwa kutosimamia kikamilifu zoezi hilo na kusababisha ucheleweshaji wa kukamilisha mradi katika maeneo yao.

“Huku ambako jamii imeshiriki vizuri miradi imekamilika vizuri lakini huku ambako jamii haijashiriki miradi imesuasua, kuna maeneo waratibu elimu alifika mara moja tu mpaka mradi unakamilika hapo jamii itahamasika vipi? ni lazima musimamie miradi yote inayokuja katika maeneo yenu kwa kuwashirikisha wananchi”, alifafanua Mkuu wa Wilaya.

Hata amewataka watendaji ambao hawajafanya vizuri kwenda kufanya maboresho ya maeneo ambayo hayajakaa vizuri ili kuikamilisha miradi yao huku akisisitiza kuishirikisha jamii na yenyewe ishiriki kuchangia miradi hiyo pamoja na mingine inayojitokeza kwa kuwa wao ndio wanufaika wakubwa.

Kwa upande wake Ofisa Elimu Sekondari wa halamshuri hiyo Mwl. Athumani Salumu, amesema kuwashirikisha wananchi kwenye kuimarisha miundombinu ya shule sio kosa jambo hilo lipo kisheria, waraka namba 3 wa mwaka 2006 wa elimu msingi bila malipo, umeruhusu  jamii yote kuchangia kuboresha miundombinu ya shule hivyo pale palipo na maradi wanachi washirikishwe.

Naye Ofisa Elimu Msingi Mwl. Mohamed Mwende, amesema lengo la halamshauri ni kumaliza tatizo la matundu ya vyoo hivyo nimatarajio yao mpango huo utafanikiwa kuwa serikali imewapunguzia mzigo mkubwa kilichopo ni kujipanga kikamilifu ili kukalisha azma yao na ni imani yao watafanikiwa.

Kampeni ya shule ni choo imeasisiwa na Mkuu wa Mkoa Mtwara Gelasius Byakanwa, na inatekelezwa katika mkoa wote wa Mtwara ikilenga kuondoa tatizo la matundu ya vyoo kwa walimu na wanafunzi wawapo shuleni, kuwaondelea adha na kulinda afya zao, ambapo wilayani Newala mkuu wa wilaya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ndiye anayewezesha vitendea kazi kwenye shule zinazotekeleza kampeni hii.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa