• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Mji Newala yashauriwa kuwekeza katika elimu ya matumizi ya mfumo wa TAUSI

Posted on: March 8th, 2023

Afisa Usimamizi wa Fedha mkoa wa Mtwara Bi. Upendo  Muze amewaomba watendaji wa Halmashauri ya Mji Newala kuwekeza kwenye mfumo mpya wa ukusanyaji wa mapato  wa TAUSI  na kuwaelimisha watumiaji ambao ni walipakodi juu ya faida za mfumo huo.

Ameyasema hayo kwenye semina elekezi ya matumizi ya mfumo wa TAUSI kwa wakuu wa idara na watendendaji wa Kata na Vijiji wa Halmashauri hiyo iliyofanyika Machi 5, 2023 kwenye ukumbi wa mikutano Halmashauri.

Bi. Muze ameeleza kuwa  mfumo wa TAUSI utamuwezesha mlipa kodi na  mkusanya mapato wa ngazi ya chini kutosumbuka kuomba namba ya malipo kwa kwenda ofisini badala yake umetengenezewa mazingira wezeshi ya mteja  kujiihudumia mwenyewe popote alipo kwa kutumia mtandao wa mawasiliano.

 “Manufaa ya mfumo mpya wa tausi kiukweli ni mfumo mzuri na nirahisi, na mfumo huu wa TAUSI kwa sasahivi unamuwezesha yule anaekusanya mapato kuomba namba ya malipo au control number bila kufika huku ofisni,  yaani anaweza kujihudumia mwenyewe huko aliko ili mradi awe na network.” Alieleza Afisa usimamizi huyo.

Aidha Muze amesema utendaji kazi wa mfumo huo ni mzuri hivyo ameiomba Halmashauri ya mji Newala kuwekeza katika utoaji  elimu  ili kuwezesha matumizi sahihi ya mfumo huo wa ukusanyaji wa mapato kwa njia ya mtandao kupita mashine za ukusanyaji mapato kielektroniki (POS).

Nae  Mtunza Hazina wa Halmashauri hiyo Bi. Costantina Shao anasema lengo la Serikali ni kuhakikisha mashine zote za kukusanyia mapato zinafanya kazi kwa kutumia mfumo wa TAUSI ambapo katika halmashauri yake mpaka mwezi  Februari 2023 jumla ya POS 28 zimeshasajiliwa kwenye mfumo na lengo ni kusajili mashine 48 hadi kufikia mwezi Aprili 2023.

Hata hivyo Shao ameipongeza Serikali kwa kuleta mfumo wa TAUSI kuwa unakwenda kupunguza gharama mbalimbali za uendeshaji kama za uchapishaji wa risiti za malipo ambazo zilikua zitumia karatasi nyingi sambamba na kupunguza gharama kwa mlipa kodi na mkusanyaji wa mapato kwa kuwa huduma itatolewa mahali walipo pamoja na udhibiti wa upotevu wa mapato wakati wa ukusanyaji na ulipaji wa kodi.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa