• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

HOSPITALI YA WILAYA YA NEWALA IMEANZA KUTOA MATIBABU YA VIUNGO KWA NJIA YA MAZOEZI

Posted on: July 1st, 2025

Wananchi wenye matatizo ya kiharusi, mifupa na watoto waliochelewa katika hatua za ukuaji wa halmashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara wametakiwa kutowaficha wagonjwa na badala yake wajitokeze kupata matibabu kwa njia ya mazoezi.

Wito huo umetolewa na mtaalam wa viungo katika Hospitali ya wilaya Newala Ndg. Markus Lugenge ambaye amebainisha kuwa serikali imeshaleta vifaa tiba hospitanini hapo na tayari huduma imeshaanza kutolewa.

‘’Huduma yetu tumeanza pale ambapo vilipofika vifaa, huduma hii inahusisha wale watu wenye matatizo ya stroke yaan kiharusi, watu wenye shida ya mgongo, kiuno hadi kwenye shingo pia wanaosumbuliwa na shida mbalimbali katika miguu na kushindwa kutembea na watoto ambao wamechelewa hatua za ukuaji”. Ameeleza

Lugenge amesema serikali imetanua wigo wa upatikani wa huduma hiyo ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma karibu na maeneo yao kwa kuwa awali huduma hizo zilikua zinatolewa kwenye hospitali bingwa, za kanda, mikoa pamoja na baadhi ya hospitali za wilaya.

Hata hivyo mtaalam huyo amesema watu wenye changamoto hizo wasipopata ufumbuzi wa shida zao hali ya utegemezi inaongezeka kwenye jamii hivyo ni wakati wa kuchukua hatua ya kukabiliana na tatizo hilo kwa kuwapatia matibabu sahihi.

“Kama kuna watoto wamepata matatizo ukubwani au walizaliwa na hiyo hali, ningependa kuwahusia wananchi kuwa wasikae nyumbani na watu wenye matatizo ya viungo kwani matatizo kama haya yanaongeza utegemezi katika jamii’’. Amefafanua mtaalam huyo wa viungo

Aidha kwa uapande wake Bi. Mariam Mnemwa mmoja wa wananchi wanaopata matibabu hayo ameishukuru serikali kwa kusogeza karibu huduma ya mazoezi kwakuwa walikuwa wanasafiri kwenda hospitali ya Ndanda au Mtwara ambako walikuwa wanatumia gharama kubwa za usafiri, malazi pamoja na chakula.

“Huduma hii walipotusogezea karibu tunaishukuru serikali kwasabu kila wakati tulikuwa tunaipata mbali tunapata shida pakulala pia nauli unaweza kwenda kwa mwezi mara moja au mara mbili kwahiyo serikali S izidi tu kutuongezea vifaa’’. Alieleza Bi. Mariam

Hospitali wa wilaya ya Newala ambayo ipo chini ya Halmashauri ya Mji Newala ilianza kutoa huduma ya mazoezi kwa wagonjwa wa viungo mwezi Aprili, 2025 mara baada ya kupokea vifaa tiba kutoka serikali kuu.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA NEWALA IMEANZA KUTOA MATIBABU YA VIUNGO KWA NJIA YA MAZOEZI

    July 01, 2025
  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa