• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Idara ya kilimo Newala Mji yawataka vijana kujitokeza kilimo cha umwagiliaji

Posted on: September 4th, 2019

Idara ya kilimo ya halmashauri ya mji Newala imewataka vijana kujitokeza kwenye kilimo cha umwagiliaji kwa kuwa halmashauri hiyo inalo eneo kubwa lenye miundombinu ya umwagiliaji na wao ndio nguvu kazi ya Taifa kuelekea uchumi wa kati wa viwanda.

Hayo yameelezwa leo Jumatano 04/09/2019 na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Bw. Calistus Komba wakati anaelezea wajibu wao kwa vijana wanaojishughulisha na kilimo ambapo ameeleza kuwa jukumu lao kubwa ni kuwawezesha kwenye mafunzo ya kitaalam ya kilimo bora pamoja na kuwashauri kwenye masuala ya masoko.

Komba amewataka vijana kujitokeza kwa wingi kwenye kilimo kwa kuwa halamashauri hiyo inalo eneo kubwa lenye miundombinu bora ya umwagiliaji iliyowekwa na serikali kupitia wahisani, likiwamo bonde la Lipeleng’enye lililopo Kijiji cha Chihanga Kata ya Mkunya lina hekta 190 na bonde la Chikwedu Chipamanda lililopo Kata ya Mcholi 1 lina hekta 1200 ambayo hayatumiki ipasavyo kwa kukosa watu wa kilima.

Hata hivyo amesema halamashauri hiyo ina vikundi 12 vilivyotambuliwa, vinavyojishughulisha na kilimo lakini kikundi cha Uvumilivu kilichopo Kata ya Makote ni cha kuigwa kwa kuwa vijana wanazalisha mazao mengi ya mbogamboga na ufugaji wa samaki kwa nguvu zao na idara ya kilimo iliamua kuwaunga mkono kwa kuwapatia utaalamu wa kilimo cha kisasa ili wazalishe kwa tija.

Katika hatua nyingine amewataka vijana kutambua kilimo kinafaida na kwakuzingatia sera na mipango ya serikali kwenye kilimo, wigo wa soko la bidhaa za kilimo umezidi kutanuka, kwani licha ya mazao ya Korosho na Ufuta ambayo yapo kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani lakini mazao ya Muhogo na Mbaazi yamepatiwa wanunuzi wa uhakika kwa msimu wa mwaka 2019.

Kwa upande wao vijana wa kikundi cha Uvumilivu kinachojihusisha na shughuli za kilimo cha ustani wameishukuru halmasahauri ya mji Newala na serikali kwa ujumla kwa kuwaunga mkono katika shughuli zao za uzalishaji na kuahidi kuendelea kujiimarisha zaidi katika uzalishaji kwa kuwa wanalo eneo la kutosha.

Kikundi cha Uvumilivu, kipo Kijiji cha Makote Kata ya Mkote halmashauri ya mji Newala, kina wanachama tisa (9) na eneo la ekari sana (7), mpaka sasa wamelima Nyanya, Bamia, Chainizi, Mchicha, Kabeji, ufugaji samaki na wanendelea na ujenzi wa banda la kufugia kuku.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa