• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Idara ya kilimo yatoa elimu kwa mawakala wa uuzaji mbolea ya kukuzia (UREA) kuhusu bei elekezi

Posted on: October 24th, 2019

Idara ya kilimo halmashauri ya mji Newala, leo Alhamisi tarehe 24/10/2019 imekutana na mawakala wa uuzaji Mbolea waliopo ndani halmashauri hiyo, kwenye kikao cha pamoja cha kupeana uelewa wa agizo la serikali kuhusu bei mpya elekezi ya ununuzi na uuzaji wa mbolea ya kukuzia (UREA).

Akizungumza katika kikao hicho, kaimu mkuu wa idara hiyo Ndg. Nelson Mtunga, amesema Serikali kupitia wizara ya kilimo imeshatoa mwongozo wa bei ya mbolea kuanzia kwa wasambazaji, mawakala na mkulima kwa lengo la kumlinda wananchi na unyonyaji wa kuuziwa bidhaa hiyo gharama kwa kubwa isiyoendana na uzalishaji wake.

Mtunga amafafanua kuwa agizo hilo limetolewa kwa kuzingatia uzalishaji na faida ya mfanyabiashara pamoja na mkulima na tathmini hiyo imefanywa na Mamlaka ya udhibiti mbolea nchini (TFRA), kwa mamlaka waliyonayo na katika eneo la halmashauri ya mji Newala bei elekezi ya kuuza inatakiwa isizidi Tsh. 52,929/= kutokana na mawakala wake kuwa na mitaji midogo ya kuagiza mbolea chini ya tani kumi.

Aidha amefafanua kuwa, gharama za uuzaji na kununua zinatofautiana kutokana na kiasi kinachonunuliwa na umbali lakini hairuhusiwi kuuza juu ya bei elekezi na endapo kutakuwa na changamoto yoyote, mawakala wawasiliane na kamati ya pembejeo ya wilaya ili washauriane na kupata ufumbuzi wa pamoja na si mfanyabiashara kuamua mwenyewe.

Kwa upande wao mawakala walioudhuria kikao hicho, wameipongeza hatua hiyo ya serikali kuwa ni ya muhimu kwani inatengeneza ukaribu wa utendaji kazi na wamefurahishwa kuona maombi yao ya kuleta pembejeo mapema kwa mwaka huu yamesikilizwa hivyo wamesisitiza ushirikiano huo uimarike zaidi na pale zinapojitokeza changamoto zipatiwe ufumbuzi vizuri, ili kufikia malengo ya pamoja.

Baadhi ya mawakala hao Bw. Mkumba Bakaari na Azim Muhibu wameshauri kuwa, pamoja na uamuzi nzuri wa serikali wa kutoa mwongozo wa bei, lakini pia iingilie kati suala usafirishaji na kutoa mwongozo kwani ipo changamoto kubwa ya wasafirishaji kujipangia gharama wanazotaka wao bila kuangalia hali halisi ya biashara.




Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa