• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mbio za Mwenge wa Uhuru, zaridhishwa na miradi ya mandeleo Newala mji

Posted on: October 3rd, 2019

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2019 Mzee Mkongea Ali, amesema ameridhishwa miradi ya maendeleo ya halmshauri ya Mji Newala na kwamba mbio hizo nitaendelea kumuenzi baba wa Taifa kwa kufanya kazi bila kuchoka, kupinga rushwa kwa vitendo pamoja na kupiga vita ujinga, maradhi na umasikini.

Ameyasema hayo leo Alhamisi tarehe 03/10/2019 alipokuwa anaongea na wananchi wa halmashauri ya mji Newala, waliojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru kwenye maeneo tofauti ya miradi ya maendeleo, nakueleza kuwa serikali imeamua kutekeza hayo kupitia falsafa ya serikali ya awamu ya tano ya hapa kazi tu.

Mkongea amesema mwenge wa uhuru unapaswa uenziwe kwa kuendeleza fikra za muasisi wake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyetaka wananchi wote wapate haki zao za msingi kwa kuzingatia nidhamu ya uwajibikaji na uadilifu katika matumizi ya fedha za umma na utumishi bora makazini.

Aidha kiongozi huyo amesema ameridhishwa miradi yote ya halmshauri hiyo ikiwemo klabu ya wapinga rushwa shule ya sekondari Mtangalanga, Zahanati ya Tupendane, Madarasa ya shule ya sekondari Newala, Ujenzi wa barabara ya lami ya kimomita moja (1km), shughuli za vikundi vya ujasiriamali pamoja na utunzaji wa chanzo cha maji cha Mkunya.

Kwa upande wake  Mbunge wa jimbo la Newala mjini ambaye pia ni Waziri wa utumishi na utawala bora Mhe. George Mkuchika amefurahishwa na klabu ya wapinga rushwa kwa kuwa klabu hiyo ni ya wanafunzi na wameokana kuelewa vizuri athari za rushwa hatua ambayo ianaonyesha kuwa itatoa mchango mkubwa wa kupambana na rushwa nchini.

Aidha Mhe. Mkuchika amesema kama nchi itashamiri vitendo vya rushwa haiwezi kuwa na maendeleo kwa kushindwa kukusanya kodi, ndio maana baada ya Rais John Magufuli kuingia madarakani na kudhibiti mianya ya rushwa maendeleo yamekuwa kasi kubwa kwani makusanyo ya uhakika yanafanyika na fedha kupelekwa kwenye miradi ya wananchi.

Hata hivyo viongozi hao kwa pamoja wamewataka wananchi kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kujiandikisha, kugombea na kupiga kura kama inavyosisitiza kaulimbiu ya mbio za mwenge 2019 kwa uongozi bora kwenye ngazi ya kijiji, mtaa na kitongoji ndio kiungo muhimu cha maendeleo katika jamii.

Kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru 2019 inasema “Maji ni haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa”.


Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa