• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mhe. Mckuchika amesema Serikali itaendelea kupelekea maendeleo kwa wananchi

Posted on: July 14th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini Mhe. George Mckuchika amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuwapelekea maendeleo wananchi wake.

Ameyasema hayo akiwa kwenye ziara yake ya kuongea na wananchi kupitia mikutano ya hadhara kwenye kata zote 16 za jimbo hilo kuelezea hatua zilizofikiwa za utekelezaji wa ahadi za serikali za kuleta maendeleo kwa watu.

Mhe. Mkuchika ameeleza kuwa ipo miradi mikubwa inayoendelea kutekelezwa na serikali jimboni humo ukiwemo mradi wa ukarabati miundombinu ya maji wenye thamani ya shilingi bilioni 84 pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara ya Mnivata Masasi kwa kiwango cha lami unaogharimu shilingi bilioni 238.

Miradi mingine ni mradi wa usambazaji umeme vijijini REA ambao umelenga kufikisha umeme kila kijiji ifikapo mwezi disemba mwaka huu, ujenzi wa vituo viwili vya afya Nambunga na Nanguruwe ambavyo tayari vimeanza kutumika.

“Kwa hiyo mimi nawaomba watu wa Newala tumpongeze Rais Samia na serikali yake kwa kazi hii nzuri ambayo imeanza”. Alieza Mkuchika

Aidha katika hatua nyingine ameeleza hatua ya utekelezaji wa ahadi yake kuunganisha mji wa Newala na Mkunya kwa lami ambapo amesema kuwa hatua za ujenzi wa barabara ulishaanza na zaidi ya kilometa sita zimeshajenga na hivi karibuni kilometa mbili zingine zitaanza kufanyiwa kazi.

“Mimi katika kampeni ya mwaka 2020 nilisema nipeni miaka mitano nataka niunganishe mji wa Newala na Mkunya kwa lami, tayari nimeanza nimehafikisha lami makondeko na mwaka tumepata lami kilometa mbili tunatoa lami kutoka Makondeko mpaka Kiuta na mwakani tutaitoa Kiuta mpaka kituo cha Afya Mkunya”. Alifafanua mbunge huyo.

Akiwa katika ziara hiyo pia Mhe. Mkuchika alitembelea ujenzi wa kituo kipya cha Polisi Kiuta chenye thamani ya shilingi milioni ya 150 fedha kutoka serikali kuu, ambapo wananchi wa Tarafa ya Mkunya kupitia diwani wao wamemshukuru mbunge jitihada zake za kuiomba serikali kuwapatia kituo hicho.

“Kwa kwali tulikuwa tunapata tabu kupeleka mambo yetu ya kiusalama Polisi kwa kuwa kituo kipo mbali hivyo gharama ilikuwa kubwa lakini ujenzi wa kituo hiki utatusaidia ukizingatia mahakama tayari tunayo hapa hapa tunaishukuru serikali na wewe mbunge kwa kutusemea”. Alieleza diwani wa Kata ya Mkunya Mhe. Karani.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa