• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mhe. Mkuchika aikabidhi Nangwanda Sekondari msaada wa kompyuta na printa vyenye thamani ya shilingi milioni 13

Posted on: March 25th, 2020

Mbunge wa jimbo la Newala Mjini Kapt. Mstahafu Mhe. George Mkuchika leo Jumatano Machi 25, 2020 amekabidhi msaada wa kompyuta 5 na printa 1 vyenye thamani ya shilingi milioni 13.3 katika shule ya sekondari Nangwanda huku akisisitiza kuendelea kusaidia maendeleo ya jimbo hilo kwa vitendo.

Mhe. Mkuchika mbaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumushi wa umma na utawala bora amesema anawashukuru Mfuko wa Mawasiliano Kwa Wote (UCSAF) kwa kukubali ombi lake la kupatiwa vifaa hivyo kwa ajili ya wananchi wa jimbo hilo hasa shule hiyo ya wasichana yenye kidato cha kwanza mpaka cha sita.

Aidha amesema yeye kama Mbunge atahakikisha anawasemea wananchi wa Newala kwa serikali na wahisani mbalimbali ili kukabiliana na baadhi changamoto zilizopo na kuweka wazi kuwa ameshaongea na kupatiwa msaada wa madarasa sita na Mamlaka ya Elimu Nchini (TEA) pamoja na madarasa mengine sita kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.

Hata hivyo Mhe.  Mkuchika ameeleza kuwa katika msaada wa madarasa sita kutoka mamlaka ya elimu madarasa matatu yatajengwa sekondari ya Nambunga kwa kuwa wanatarajia kuanzisha kidato cha tano na sita kwa wafulana na madarasa mengine matatu tatajengwa  shule ya sekondari George Mkuchika na madarasa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu matatu yatajengwa sekondari ya Makote na matatu mengine Shule ya Msingi Nangawala leongo likiwa ni kuongeza madarasa ya shule hiyo na mwakani ianze kupokea wanafunzi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala Ofisa Elimu Sekondari Mwl. Athuman Salum ameshukuru Mbunge kwa msaada huo ambapo amempongeza kwa kuwa mstari wa mbele kuisaidia halamshauri na kwamba hiyo si mara yake ya kwanza na msaada huo utasaidia sana katika hatua za kujifunza na kufundisha kwa wanafunzi na waalimu pamoja na kuondokana na hoja za matumizi ya fedha za serikali kwa kutumia mfumo FAARS anaohitaji matumizi ya kompyuta.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Mwl. Beatrice Marwa amesema wanamshukuru sana mheshimiwa Mbunge kwa kuwa walikua na uhitaji mkubwa wa kompyuta za waalimu kwa ajili ya kufundishia kwa kuwa malighafi nyingi za kufundishia kwasasa zinapatikana mtandaoni na hata kwa wanafunzi kwa hiyo kwa shule ni ukombozi na kuwaomba wadau wengine wenye uweze wakusaidia wajitokeze kwani bado wanao uhitaji mkubwa wa kompyuta ili kwenda sambamba na mfumo wa elimu yasasa.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa