Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mhe. Mkuchika awataka walemavu kujitokeza kuomba mikop ya halmashauri

Posted on: February 24th, 2020

Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini Mhe. George Huruma Mkuchika amevitaka Vikundi vya ujasiriamali vya walemavu kujitokeza kuomba mikopo ya vijana, wanawake na walemavu inayotolewa na serikali kupitia halmshauri  ili waweze kunuifaka nayo na kupiga vita umaskini.

Ameyazungumza hayo mjini Newala siku ya  jumamosi  22/02/2020 katika wa hafla ya kukabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 67.5 kwa vikundi 27 vya vijana wanawake na walemavu viliovyoomba mkopo halmashauri ya mji Newala, ambapo katika taarifa ya utekelezaji ya afisa maendeleo ya jamii ilionyesha uwepo wa uhaba wa vikundi vya walemavu vinavyojitokeza kuomba mikopo hiyo.

Aidha Mhe. Mkuchika ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala Bora, amesema utoaji wa mikopo hiyo ni mpango wa serikali na sera ya Chama Cha Mapinduzi, kuendeleza wazo la Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere la kupiga vita ujinga, maradhi na umaskini.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Afisa Elimu Sekondari Mwl. Athuman Salum, amesema tangu halmashauri hiyo ilipoanza kutoa mikopo mwaka 2016/2017 mpaka disemba 2019 imeweza kukusanya zaidi shilingi bilioni 3 na milioni 900 na asilimia 10 ya fedha hizo zimekopeshwa kwa vikundi kama agizo la Mhe. Rais na muongozo wa serikali unavyotaka.

Akiwasilisha  taarifa yake Afisa Maendeleo ya Jamii wa halmshauri ya mji Newala Bi. Frola Barakana amesema mpaka sasa jumla ya vikundi 196 na wanavikundi 1648 wameshanufaika na mpango wa serikali wa kuwezesha wananchi kunufaika kiuchumi, kwa kupatiwa mikopo hiyo isiyo na riba ambapo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 hadi disemba 2019 halmashauri imefanikiwa kutenga shilingi milioni 360.2 ikiwa ni asilimia 10 ya makusanyo yake halisi na kuelekeza kwenye vikundi vya vijana, wanawake na walemavu.

Sambamba na hilo Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani Newala Edwin Mukama, amewataka wanavikundi hao kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa za maafisa wanaowadai rushwa wakati wa hatua za kuomba mikopo kwani kufanya hivyo ni kinyume na uwajibikaji wa watumishi na maadili ya kazi yao.

Naye Afisa mwakilishi kutoka Benki ya NMB Bi. Aneth Madiwa amevitaka vikundi kuzitumia akaunti zao benki kwa kuwa hazina tozo za huduma pia zitawasidia kutambua faida na akiba wanayoipata katika mirasi yao sambamba na kuachana na  tabia ya kuzitumia kwa kupokelea fedha na kuzitelekeza.

Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, viongozi wa vijana, wanawake na walemavu wameishukuru serikali kupitia halmashauri pamoja na Mbunge kwa kuwajali na kuwapitia mkopo kwa kuwa inawasidia kutatua changamoto zao za kiuchumia kutokana na faida wanayoipata huku wakivitaka vikundi kusimamia mipango na malengo walioyojiwekea.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa