• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi awataka madiwani kuwaelisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo

Posted on: April 29th, 2020

Mkurungenzi wa halmashauri ya Mji Newala ndg. Andrew Mgaya amewaomba madiwani wa halamsahauri hiyo kutoa uelewa kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuendelea kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo yao na kuachana na dhana kwamba miradi hiyo haiitaji nguvu za wananchi.

Ameyazungumza hayo siku ya Jumatatu Aprili 27, 2020 katika mkutano wa baraza la madiwani wa robo ya tatu 2019/2020 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo ambapo mkurugenzi huyo, ameeleza kuwa baadhi ya maeneo wananchi wamekuwa dhana hiyo potofu.

Amefafanua kuwa miradi yote ya mandeleo inahusisha nguvu za wananchi lakini baadhi ya maeneo kwenye mradi wa ujenzi wa madarasa imejitokeza wananchi kukataa kuchangia nguvu kazi wakidai kuwa mradi huo umetengewa fedha za kukamilisha kuanzia hatua za awali hadi kukamilisha jambo ambalo si sahihi.

Akielezea hali ya mapato ya halmashauri mkurugenzi Mgaya ameeleza kuwa hadi kufikia tarehe 30 machi mwaka huu, halmashauri imekusanya shilingi bilioni 1.4 kati ya shilingi bilioni 2.1 sawa na asilimia 69.7 na kujudi zinaendeleza za kukusanya zinaendelea ili kufikia lengo kusudiwa la bajeti.

Aidha katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa Corona  amewataka madiwani hao kuwahimiza wananchi kuchukua taadhari kwa kuwa jukumu hilo halina mwenyewe ni la kila mmoja, sambamba na kuwalinda watoto wao kike na mimba wakati wa huu likizo pamoja na kuwahimiza kujisomea binafsi na kupitia runinga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mhe. Sambili Mohamedi amemuomba mkurugenzi kuwaelekeza watendaji wa halmashauri kutoa ushirikiano kwa madiwani kwani wao ndio chachu ya kutoa msukumo kwa wananchi kushiriki na kusimamia ufanisi wa miradi husika.

Katika hatua nyingine Mhe. Sambili amesisitiza ombi la mkurugenzi kwa madiwani la kuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi juu kujitolea nguvu kazi kwa kuwa kutofanya hivyo ni kuikwamisha miradi  kitu kitakachopelekea kuzorotesha maendeleo yao wenyewe.

Mkutano huo ulifanyika kwa mda mfupi kwa zingatia tahadhari zote za kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona kwa kuhusisha watu wachache, kukaa umbali wa zaidi ya mita moja, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa sabuni maji tiririka.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa