• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji ataka ulinzi wa watoto kwa kufunika visima vya maji

Posted on: May 11th, 2023

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala Bi. Shamim Mwariko amewaagiza Maafisa watendaji wa kata kuanda mpango wa kutoa elimu ya usalama wa kufunika visima vya maji kwa wananchi ili kuepusha matukio ya vifo vya watoto.

Ametoa agizo hilo Mei 09, 2023 wakati naongea na maafisa hao ofisini kwake kufuatia uwepo wa matukio ya vifo vya watoto wanaozama na kupoteza maisha yao kwenye visima vya maji visivyofunikwa na kueleza hali hiyo haikubaliki katika jamii.

Amesema usalama wa watoto kwenye jamii ni jambo la muhimu, hivyo hatua za kuwalinda watoto lazima zichukuliwe kwenye vijiji na mitaa kwa kushirikiana na viongozi wa maeneo husika kwa kuwa baadhi ya wananchi hawajafunika visima vyao na matokeo yake ni mabaya.

Mkugenizi Mwariko ameeleza “na watoto ni wengi sana wanaokufa, tunapokea taarifa hata kutoka maeneo mengine ya nchi yetu, mtoto anapotea watu wanaangaika wanasema sijui amepotea kusikojulikana, kumbe mtoto yupo humo humo nyumbani baada ya siku ngapi mnamuona mtoto amekufa anaelea juu”.

Hata hivyo amesema kwa kuwa sheria ndogo za kuwataka wananchi kuzingatia suala la kufunika visima hivyo zipo basi wale watakaopinga, sheria hizo zitumike kuhakikisha usalama wa watoto kwa kuwa hakuna mbadala wa uhai.

Hata hivyo baadhi ya kata lishachukua hauta ya kukabiliana na tatizo hilo mmoja wa maafisa watendaji Bi. Stephania Muhagama Afisa Mtendaji wa Kata ya Tulindane amesema katika kata yake wameendesha zoezi la ukaguzi na kuwachukulia hatua ya kulipa faini baadhi ya wananchi kwa kuwa elimu ya kufunika visima na matangazo yalishatolewa

Aidha Muhagama amefafanua kuwa lengo lao sio kuwataka wananchi kulipa faini bali ni kuhakikisha usalama wa kimwili na kiafya kwa kuwa hali ya maji kwenye visima visivyofunikwa inaonyesha sio salama kwa matumizi ya nyumbani.

“Maji yale ukiyaangalia tu unajua wala sio salama kwa matumizi ya mwanadamu unakuta maji yana kama ukungu wa kijani umetanda juu na wakati nwingine wadudu wamekufa wanaelea juu ya maji na watu wanayatumia hivyo hivyo, sasa ni vizuri tunachukua taadhari kwa kuwahimiza wananchi kufunika visima.” Alifafanua Bi. Stephania

Wananchi wengi wa Halmashauri ya Mji Newala wamechimba visima vya maji katika makazi yao kutokana na changamoto ya miaka mingi ya upatikanaji wa maji kutokana na wilaya ya Newala kuwa kwenye ukanda wa juu pamoja.

Hata hivyo katika kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wilaya za Newala, Tandahimba na Mtwara vijiji Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha shilingi bilioni 80 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya maji ya uhakika.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa