• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa wilaya Newala amewataka wanawake kuthubutu na kushikamana

Posted on: March 7th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Newala Alhaj Mwangi Rajabu Kundya amewataka wanawake kushikamana na kuthubutu katika kushiriki na kuwania nafasi mbalimbali za uongozi serikalini kwa kufuata mfano wa viongozi waliopo madarakani akiwemo mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.                

Ameyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani  ngazi ya halmashauri ya Mji Newala  katika kijiji cha Namiyonga Machi 04 2023, ambapo pia kwa kuzingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo “ubunifu na mabadiliko ya teknolojia ni chachu katika kuleta usawa wa kijinsia”  ambapo amewataka wanawake kutambua wanayo fursa  ya kiutendaji  sawa na wanaume kama ilivyoainishwa katika sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2007.

Hata hivyo Mhe. Mwangi  amewasisitiza wanawake kua mikopo iliyotolewa na halmashauri ya mji inalenga kuwawezesha wanawake kiuchumi kuleta usawa wa kijinsia na kukidhi haja ya serikali kama ilivyoeleza katika sera ya kuwawezesha wanawake ya mwaka 2004 hivyo waitumie ipasavyo mikopo hiyo kukuza uchumi wa familia na taifa kwa ujumla.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Hamisi Namata  amesema usawa wa kijinsia katika jamii unaanzia kwenye familia hivyo wanaume wawashirikishe wake zao katika maamuzi na mikakati ya maendeleo kwani mwanamke anamchango mkubwa katika kukuza pato la familia, na kwa kufanya hivyo kutapelekea usawa na kuondoa dhana ya mwanamke kuwa tegemezi.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli zilizofanywa na Halmashauri zinazowahusu wanawake Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Bi. Joice Israel amesema  halmashauri imewezesha jamii kuunda vikundi vya vikoba na ujasiriamali 593 ambavyo asimilia 90 ya wanachama ni wanawake

“Aidha tumetoa elimu mashuleni ya kutokomeza ukatili wa kijinsia na aina za ukatili, pia tumefanikiwa kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake 178 kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka machi 2023 vimenufaika” aliongeza Israel.

Nae mkuu wa mtandao wa polisi wanawake wilayani Newala( TPF-NET) Mkaguzi  Msaidizi Tumaini Ngwanda amesisitiza suala la ulinzi shirikishi kwa jamii katika kuwatunza watoto wa kike na wanawake kutokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia ambao kwa sasa unaendelea kushamiri,  hivyo jamii itumie mitandao ya simu kutoa taarifa kwenye mamlaka husika ili kukabiliana na hali hiyo.

Kwa upande wake Afisa elimu kwa umma kutoka taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilayani Newala Fides Didas amewataka wanawake kuwa walinzi wa familia kwa kuwashauri waume zao kuwa waadilifu kazini kwa ajili ya usalama wa familia.

Hata hivyo baadhi ya wanawake walioshiriki maadhimisho hayo wameeleza kuwa wanawake wenyewe wantakiwa kujitoa na kushiriki katika shughuli mbalimmbali kama ujasiliamali, ajira rasmi na uongozi ili kujenga jamii yenye usawa na mshikamano kama lilivyo lengo la maadhisho haya.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa