• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Wilaya Newala Mhe. Rajabu Kundya amezindua zoezi la ugawaji wa hati za kimila za mashamba 1659

Posted on: May 18th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Newala Mhe. Mwangi Rajabu Kundya Jumatano Mei 18, 2022 amezindua zoezi la ugawaji wa hati miliki za kimila 1659 wilayani humo kwa wananchi wa vijiji vya Chilangala, Mitema na Mkulung’ulu.

Aidha Mhe. Kundya amewataka wanawake kuacha kuwa wanyonge na kuweka kipaumbele cha kurasimisha ardhi yao kwa kuwa hiyo ni hatua ya kumkwamua mwanamke kiuchumi na kukuza hali ya maisha ya mtu mmoja mmoja familia na Taifa zima kwa ujumla.

Mkuu wa wilaya huyo amewasisitiza wanawake kutobaki nyuma kwenye mambo yote yanayowakomboa na kuwanyanyua kiuchumi kwa kuwa mwanamke ndio njia sahihi ya kuikomboa jamii.

Kwa upande wake aliyekuwa Mratibu wa zoezi hilo la urasimishaji ardhi vijijini kutoka Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) Ndg. Antony Temu, amewaomba wananchi waliopokea hati hizo kwenda katika kujiletea maendeleo.

Hata hivyo Temu amefafanua kuwa, kazi ya MKURABITA ni kuwajengea uwezo wananchi kwa kuwainua kiuchumi kupitia rasilimali zao ambazo awali walikuwa wakizitumia pasipo kunufaika nazo ambapo mpaka sasa tayari wameshazifikia halmashauri 63 kote nchini.

Akizingumza kwa niaba ya wakurugenzi wa halmashauri za Wilaya na Mji Newala Ofisa Ardhi na Maliasili wa halmashauei ya wilaya Newala Bi. Magreti Likonda amewashukuru MKURABITA kwa uratibu na kuwawezesha wananchi ambao sasa jukumu limebaki kwao kuchukua hatua za kunufaika na hati hizo.

Naye Mratibu wa zoezi hilo halmashauri ya mji Newala Ofisa Ardhi Ndg. Salvatory Nginga amesema pamoja na mafanikio hayo yaliyofikiwa lakini zilikuwepo changamoto kadhaa ikiwemo kijiji kulikuwa hakijapimwa na hakikua na cheti cha ardhi ya kijiji hivyo mpango huu uliwezesha kutatua changamoto hiyo.

Baadhi ya wananchi waliopokea hati hizo Ndg. Jafo Nandonde na Rashid Machemba wameishukuru serikali na waratibu wa mradi kwa kuwa sasa ni kama wameshafunguliwa mlango kuelekea hatua za maendeleo kupitia rasilimali ardhi.

Katika mradi huu uliohusisha vijiji vitatu wilayani Newala, jumla ya hati miliki za kimila 913 zimetolewa halmashauri ya wilaya Newala, kijiji cha Chilangala hati 494 na kijiji cha Mitema hati 419 wakati halmashauri ya mji Newala ikuwa na kijiji kimoja cha Mkulung’ulu ambacho kimepata hati 746.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa