Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mwenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa waapishwa leo tayari kuanza majukumu yao

Posted on: November 27th, 2019

Mwenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa wa halmashauri ya Mji Newala, walioshinda kwenye uchaguzi uliofanyika Novemba 24, mwaka huu, leo wameapishwa tayari kwenda kutekeleza majukumu yao ya kuwatumikia wananchi na serikali.

Hafla hiyo imefanyika leo Jumatano Novemba 27, 2019, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya mwanzo Myambe-Newala Bi. Devotha Salumu, ambaye amewataka kuzingatia viapo walivyokubali kiapo cha uaminifu pamoja na kiapo cha utii na uadilifu.

Akizungumza mara baada wa kuapishwa viongozi hao wapya, Mkuu wa wilaya Newala Bi. Aziza Mangosongo amewataka kutambua jukumu walilonalo ni kubwa hivyo umoja unahitaka ili kufanikisha malengo ya serikali na kuwatumikia wananchi waliowachagua na kuwataka kuondoa makundi yote na kuimarisha umoja baina ya vyama na wananchi wao.

Aidha Mkuu wa wilaya amewata kutokumbatia madaraka na badala yake washirikiane kikamilifu na wananchi wao kupitia vikao halali kuibua na kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika mitaa yao na kuepuka kujigeuza miungu watu kutokana na madaraka waliyonayo.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Mkoa Mtwara anayeshughulikia serikali za mitaa Bw. Nuru Ringo amewataka wenyeviti kuzingatia kanuni, kuitisha mikutano ya halamshauri ya mitaa kwa mujibu wa kanuni, kuwapa wananchi taarifa za mapato na matumizi pamoja na kuwa na msimamo wakati wa kusuluhisha migogoro kwa  maslahi ya pamoja.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Newala Bw. Mussa Ramadhani Mwevi, amewapongeza viongozi hao, ambao wote wametokana na CCM na kuwataka kwenda kutekeleza majukumu yao kwa kushirikiana na watendaji wa serikali katika kuwatumikia wananchi na kuachana na kubaguana.

Akitoa taarifa ya mafanikio ya uchaguzi huo, Msimamizi wa uchaguzi halamashauri ya mji Newala Bi. Sophia Makungu amesema kulikua na vituo 189 vya kupigia kura na vyama vitatu CCM, CHADEMA na CUF vilishiriki uchaguzi huo, huku mitaa miwili pekee ndio ambayo iliingia kwenye mchakato wa kupiga kura na maeneo mengine wagombea wakipita bila kupingwa na kwenye matokeo ya jumla Chama Cha Mapinduzi kimeshida viti vyote.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa