• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Newala Day yaweka mikakati wa kuondoa sifuri kidato cha nne na cha pili

Posted on: July 15th, 2020

Shule ya Sekondari Newala iliyopo Halmashauri ya mji Newala, imeweka mkakati kufanya vizuri na kuondoa daraja sifuri na kuongeza ufaulu wa daraja la kwanza mpaka la tatu kwa wanafunzi watakaofanya mtihani wa kidato cha nne na cha pili mwaka huu 2020.

Hayo yamebainishwa leo Jumatano Julai 15, 2020 na Mkuu wa shule hiyo Mwl. Briton Limbe wakati anaelezea mipango iliyokwa na shule yake kwa ajili ya kuongeza ufaulu wa wanafunzi wanaofanya mitihani, “Sisi kama shule tayari tumeshaweka mkakati wa kufundisha mbinu za ziada kwa masomo ambayo wanafunzi wanayaona ni rahisi ili tuwatie moyo na kuwaongezea maarifa ya kufanya mitihani kwa kujiamini ili waondokane na F”, ameeleza Mkuu huyo.

Amesema wameyaangalia masomo manne ambayo wanafunzi huwa wanayapenda ambayo ni Kiswahili, Kiingereza, Uraia na Historia ambayo kama wakiwajengeza uwezo kikamalifu na kuwaelekeza maeneo muhimu ya kuzingatia, wanafunzi atapata alama nzuri na kuondokana na ziro.

Aidha Mwl. Limbe ameutaja mkakati mwingine ni kuwa na muda ziada wa masomo na kutoa msaada kwa wanafunzi wenye uwezo mdogo, kufanya mitihani kila mwisho wa wiki yenye hadhi ya Taifa ili wanafunzi wapate picha halisi ya mitihani hiyo pamoja na kuhamasisha wazazi kuwahiza watoto wajisomee wakiwa nyumbani na kuchangia chakula ili wapate chakula wawapo shuleni.

Kaka Mkuu wa shule hiyo Ayubu Issa Zefania anayesoma kidato cha nne amesema wao kama wanafunzi wameopokea mkakati huo kwa mikono miwili kwa kuwa wanaamini mwanafunzi akifanya mazoezi mara kwa mara lazima atapata ufaulu nzuri na zaidi wanazingatia nidhamu kwani ndio msingi wa mafanikio yao.

Kwa upande wake Nulfa Omary wanafunzi wa kidato cha pili amesema mkakati huo umewapa hamasa kwa kuwa walikaa muda mrefu nyumbani na muda uliobaki kuelekea kufanya mitihani ni mchache hivyo anawaomba wazazi wawaunge mkono kwa kuchangia chakula ili muda wao mwingi wadumu shuleni kwani ndiko wanakopata msaada wa kieleimu na anaamini wanafunzi wengi wawapo nyumbani hawasoni.

Shele hiyo katika mtihani wa mwaka jana 2019 kitado cha nne ilifaulisha kwa zaidi ya 70% na kidato cha pili  zaidi ya  80%  na kwenye mkakati wao wasasa wamedhamiria kufikia ufaulu wa asilimia 100%.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa