• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

Posted on: August 1st, 2023

Serikali imesema kundi la wanawake na vijana likiwekewa mazingira mazuri ya uzalishaji katika shughuli za kilimo, litasaidia kufikia malengo ya taifa ya kuwa na kilimo endelevu cha kibiashara kinachokua kwa asilimia 30 hadi ifikapo mwaka 2030.

Hayo yameelezwa Agosti 01,2023 na Naibu waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Jumanne Sagini (Mb) wakati anafungua maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini katika viwanja vya Ngongo-Lindi ambapo amesema kaulimbiu ya mwaka huu imetambua umuhimu wa kundi hilo katika uzalishaji wa chakula kwenye kaya.

Aidha Mhe. Sagini ameeleza kuwa maonesho ya Nanenane yatumike kuchochea hamasa ya wananchi kuongeza kipato kupitia kilimo, ufugaji na uvuvi pamoja na kujifunza fursa za kuongeza ajira, upatikaji wa rasilimali mbalimbali, uzalishaji, uongezaji wa thamani na masoko.

Katika hatua nyingine amesema serikali haitavumilia machafuko yoyote yanayoweza kuondoa utulivu na amani iliyopo na kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama hususani jeshi la Polisi kudhibiti viashiria vya uvunjifu wa amani kwa haki na usawa, kufuatia migogoro ya wafugaji na wakulima iliyoanza kuibuka mkoani Lindi.

Mwenyekiti wa maonesho hayo Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi. Zainab Telack amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia wakulima wa korosho pembejeo za bure pamoja na waafisa ugani pikipiki kwa ajili ya kuongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo na mifugo.

Amesama mikoa ya Lindi na Mtwara inajivunia kuwa na ardhi yenye rutuba, madini, gesi, misitu ya asili, mbuga za wanyama, bahari, maeneo ya historia pamoja na kuwa vinara wa uzalishaji wa mazao ya korosho na ufuta yanayoingiza fedha nyingi kwenye pato la taifa.

Aidha Mhe. Telack amewaalika wawekezaji katika mikoa hiyo na kueleza kuwa hilo ni eneo muhimu kwa uwekezaji katika sekta mbalimbali za kiuchumi na inatarajiwa kuwa uchumi wa taifa utabebwa na mikoa hiyo baada ya miaka michache.

Maonesho ya wakulima nanenane kanda ya kusini yanahusisha mikoa ya Lindi na Mtwara nakufanyikia katika viwanya vya Ngongo-Lindi mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo “Wanawake na Vijana ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula”.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa