• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Serikali yawataka wakulima wa Lindi na Mtwara kulima mazao mchanganyiko soko lipo

Posted on: August 9th, 2019

Naibu waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba amewataka wakulima wa mikoa ya Lindi na Mtwara kutumia fursa ya udongo wenye rutuba kulima mazao mchanganyiko ili kuongeza kipato kwa kuwa serikali imeshaweka mazingira mazuri ya soko la uhakika kwa bidhaa za mazao.

Mhe. Mgumba ameyasema hayo jana 08/08/2019 wakati anawahutubia wananchi  na wakulima waliohudhuria kwenye kilele cha maonesho ya sikukuu ya wakulima Nanenane kanda ya kusini yaliyofanyika katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi ambapo amesema ardhi ya mikoa hiyo inafaa kwa kilimo cha mazao mengi hivyo ni wakati wakuacha kutegemea zao moja.

Aidha ameeleza kuwa serikali tayari imeshatafuka soko la uhakika kwa mazao ya ufuta, mbaazi na korosho hivyo ni suala la mkulima kuongeza juhudi kwenye uzalishaji, huku akitoa uhakika wa ununuzi wa zao la korosho kwa msimu wa 2019/20120 kwani zilizopo maghalani zote zimepata mnunuzi na muda mfupi zitaondolewa kwenye maghala yote nchini.

Sambamba na hilo amesema kauli mbiu ya mwaka huu isemayo “Kilimo, Mifugo na Uvuvi Kwa Ukuaji Wa Uchumi wa Nchi” imezingatia mchango wa sekta ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo nchini, kwa pamoja vinachangia asilimia 65% ya malighafi za viwandani nchini, asilimia 75 ya ajira, asilimia 35  pato la Taifa na asilimia 30 fedha za kigeni hivyo huu ndio muhimili muhimu wa kufikia maendeleo ya nchi.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya kudumu ya mbunge ya Kilimo, Mifugo na Maji mbunge wa Namtumbo Mhe. Edwin Ngonyani akimwakilisha  mwenyekiti wa kamati hiyo amesema kamati inaitaka wizara kupitia idara ya masoko kuongeza jitihata za kutafuta masoko ya mazao ya wakulima badala ya kuitegemea wizara ya viwanda na biashara pamoja na masoko ya walioanzisha viwanda vidogo vidogo.

Aidha katika utangulizi wa ujumbe wa wizara ya kilimo kupitia kwa mwakilishi wa katibu mkuu, amewataka wakulima kuzingatia mashariti ya matumizi sahihi ya viwatilifu kwa kuwatumia wataalam wa kilimo kwa kuwa lengo la serikali ni kuuza bidhaa za kilimo nje ya nchi hivyo ni lazima uzalishaji ukafanyika kwenye viwango bora vinavyohitajika. 

Akizungumza na wananchi walioudhuria kilele cha sherehe hizo, Mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne (Mb) Mama Salma Kikwete amewataka wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kutumia maonesho hayo kama chachu ya kuongeza uzalishaji na hatimae kufikia maendeleo kwa kuzingatia sera ya Taifa ya kuelekea uchumi wa kati wa viwanda kutokana na rasilimali zilizopo ndani ya mikoa hiyo.

Sikukuuu ya wakulima nchini huadhimishwa kila mwaka tarehe 08/08 sambamba na shamrashamra za maonesho ya wakulima na wafanyabiashara yanayofanyika kwenye kanda mbalimbali na kubeba kauli mbiu ya kitaifa ambapo kwa mwaka huu kauli mbiu inasema “Kilimo, Mifugo na Uvuvi Kwa Ukuaji Wa Uchumi wa Nchi.”




Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa