• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

TBS na SIDO watoa mafunzo yakuzalisha bidhaa bora kwa wajasiriamali wenye viwanda vidogo Newala Mji

Posted on: May 15th, 2020

Shirika la Viwango vya Ubora wa Bidhaa Nchini (TBS) makao makuu kwa kushirikiana na Shirika la viwanda vidogo vidogo (SIDO) mkoani Mtwara leo Alhamisi Mei 15, 2020 wametoa mafunzo ya kuzalisha bidhaa zenye viwango vya ubora kwa viwanda vinne vya ujasiriamali vinavyozalisha bidhaa halmashauri ya mji Newala.

Afisa mwezeshaji kutoka shirika hilo Bi. Dina Lwendo, akizungumza kwenye viwanda tofauti alivyotembea mjini Newala, amesema serikali baada ya kubaini kuwa bidhaa nyingi za wajasiriamali wadogo hazina  nembo za ubora, imeagiza bidhaa zote zinazozalishwa nchini zikidhi viwango vya ubora na kuwa nembo, hivyo TBS imeamua kushuka chini kutoa uelewa kwa wazalishaji wadogo ambao wengi wao wameonekana kutokuwa na elimu ya kutosha.

Hata hivyo Bi. Lwendo amekiri kuwa bidhaa nyingi za wajasiriamali wadogo zinakosa soko la nje na hilo linadhihirika kwenye maonyesho mbalimbali ya biashara, kutokana na kutokuwa na nembo ya ubora na ndio maana TBS imeamua kutoa elimu kuanzia kwenye hatua za awali za uzalishaji ili kulinda ubora wa bidhaa tangu kiwandani na sio kupima maabara bidhaa zinazoingia sokoni pekee.

Aidha amesema ni matumaini yao kama wajasiriamali watapata elimu vizuri kwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali chini ya SIDO na halmashauri matokeo yatakua makubwa kwani bidhaa nyingi zinao ubora wa kutosha tatizo lililopo ni kuwa zinakuwa hazijathibitishwa na hilo ndilo wanalolifanyia kazi.

Kwa upande wake Afisa mwezeshaji kutoka SIDO Mtwara Bw. Kasto Tamba amewataka wajasiriamali kuipokea fursa hiyo kwa mikono miwili kwa kuwa serikali imewajali kwani imewaunganisha SIDO na TBS kufanya kazi kwa pamoja, kurahisisha uhakikia wa bidhaa, majengo ya viwanda pamoja na hatua za uzalishaji ili kuondoa mlolongo wa zoeli hilo.

Hata hiyo amesema ipo faida kubwa kwa watakaokidhi vigezo vya kupatiwa nembo ya ubora kwa kuwa serikali imetoa muda wa miaka mitatu ya awali ya uzalishaji bidhaa kutumia nembo hiyo bila malipo yoyote na malipo hayo yatafanywa na wizara ya viwanda na biashara kwa lengo la kukusaidia kuimarisha mtaji wa biashara yako.

Naye msimamizi wa vikundi vya wajasiriamali halmashauri ya mji Newala Afisa Maendeleo ya Jamii wa halmashauri hiyo Bi. Frola Barakana ameishukuru serikali kwa kuwajali wajasiriamali wadogo kwani hiyo ndio njia pekee ya kuwakomboa na kuwaimarishia mitaji yao kwa kuwa changamoto ya ubora imeyumbisha soko la bidhaa nyingi za vikundi vya wajasiriamali.

Viwanda vya wajasiriamali vilivyotembelewa vimeishukuru serikali kupitia SIDO na TBS kwa kuwaona na kuwafikia kwenye maeneo yao hiyo inaonyesha nia ya dhati ya serikali kutaka kuwakwamua kiuchumi na wao wanaenda kuyafanyia kazi maelekezo waliyopatiwa kwa kuwa nia yao ni kuwa wazalishaji wakubwa na wafanikiwe kuuza bidhaa zao nje nchi.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa