• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Ustawi wa jamii imewataka wazazi kupunguza vitendo vya ukatili kwa watoto waliopo shuleni

Posted on: July 14th, 2022

Halmashauri ya Mji Newala kupitia idara ya ustawi wa jamii imeanzisha kampeni ya kutoa elimu ya kutambua vitendo vya ukatili kwa wanafunzi waliopo shuleni wenye lengo la kupunguza vitendo hivyo na kujenga ustawi wa watoto.

Akizungumza leo 14 Julai 2022 viwanja vya shule ya msingi Karume mjini Newala baada ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule mbalimbali, Afisa Ustawi wa Halmashauri hiyo Bi. Melania Ng’itu amesema hatua hiyo inalenga kutekeleza sera ya serikali ya kupambana na ukatili kwa watoto hivyo ni wakati muafaka kwao kuwajengea uelewa waweze kuondokana na athari za vitendo hivyo.

Ng’itu amesema kutokana na maelezo ya watoto wenyewe inaonyesha kuwa katika mazingira ya  shule na nyumbani wanatendewa vitendo vya ukatili huku baadhi yao wakiwa wanavitambua na hawajui njia za kupata msaada na wengine hawana uelewa kabisa jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa mtoto na kuitaka jamii kubadilisha mtazamo kuhusu malezi ya mtoto.

Kwa upande wake mwalimu wa michezo kwa shule za msingi wa Halmashauri hiyo Mwl. Zabron Mpini amepongeza hatua hiyo ya ustawi wa jamii na kueleza kuwa matendo ya ukatili kwa watoto yanaongezeka katika jamii na athari zake ni kubwa kwa afya ya mwili na akili pamoja hatma ya maisha ya baadae ya mtoto kwa kuwa hayasahauliki kirahisi.

Aidha amewaomba wazazi kuwa waangalizi na walezi bora kwa kuwa vitendo hivyo huanzia kwenye ngazi ya familia na yanapomkuta wanafunzi yanamuondolea uelekeo katika masomo na hata michezo kwa kuumizwa ndani ya akili na kama matendo hayo hayatasemwa ni kuwaangamiza.

Shania Shabani na Exiwanda Mnamwa wanafunzi wa darasa la saba kutoka shule ya msingi Nachituro wamesema wamepata uelewa juu ya ukatili na hatua wanazoweza kuzichukua pale watakapo kutana na matukio ya aina hiyo kwa kuwa mwanzo hawakujua wapi wanaweza kupata msaada pindi matukio ya unyanyasaji yakiwakuta.

Sambamba na mafunzo hayo ustawi wa jamii imetoa zawadi ya taulo za kike na sabuni za kufulia kwa wanafunzi hao walio kwenye kambi ya michezo.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa