• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Vijana wametakiwa kuachana na fikra za mikopo midogo na badala yake watafute fursa za mikopo yenye tija kwa Taifa

Posted on: June 8th, 2022

Vijana na wanawake wajasiriamali waliopo Halmashauri ya Mji Newala, wametakiwa kufungua fikra zao na kuziona fursa zenye tija kwa Taifa zitakazoweza kuwaunganisha na kuwasaidia kufanya mambo makubwa kwa kuwa muelekeo wa Serikali kwasasa ni kutoa mikopo ya mamilioni ya shilingi kwa vikundi vya vijana, wanawake na walemavu.

Rai hiyo imetolewa Jumatano June 08, 2022 na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Shamim Mwariko wakati wa ufunguzi wa kikao cha kuwawezesha vijana kutambua fursa za kilimo na biashara na fursa zingine zilizopo kwa vijana ili kuziunganisha na mikopo inayotolewa na serikali kupitia Halmashauri.

Mkurugenzi Mwariko amewataka vijana kubalisha mtazamo wa kuchukua mkopo wa fedha ndogo kisha kugawana na kuchangishana wakati wa marejesho kwa kuwa hilo sio lengo la mikopo hiyo na kwa utaratibu huo nchi haiwezi kukuza uchumi wake.

Amesema vijana na wanawake wanatakiwa wachukue mikopo itakayo wanuafaisha wao wenyewe na ikiwezekana itoe ajira kwa wengine ili jamii yote inufaike, “baadhi yenu humu wamepokea mikopo ya milioni ishirini, baadhi yenu wamepokea mikopo ya milioni kumi na baadhi yenu wamepokea mikopo ya zaidi ya milioni tisini tungependa utaratibu huo ni kawaida,” ameeleza Mwariko.

Mwakilishi wa Taaasisi ya kimataifa ya IITA anayeshughulikia elimu kwa vijana Bi. Veronica Kebwe amesema kazi yao ni kushirikiana na Halamashauri kupitia idara ya maendeleo ya jamaii kuwawezesha vijana kuziona fursa mpya za kilimo biashara kutokana na changamoto walizonazo kwa kuzingatia mawazo yao na kuwajengea uwezo na kuwasimamia ili kufikia lengo la kuondokana na tatizo la ajira.

Kwa uapande wake Mwenyekiti wa Kamati ya huduma za jamii ya halmashauri ya mji Newala ambaye ni diwani wa Kata ya Namiyonga Mhe. Issa Mnayahe amesema kwa wale waliopata semina wanalo deni la kueneza elimu waliyopata kwa wananewala ili lengo Serikali kupitia Halmashauri la kuwawezesha wananchi litimie.

Aidha Mkuu wa idara ya kilimo wa Halmashauri ya mji Newala Bw. Calistus Komba amesema idara imejipanga kutengeneza vikundi vya wakulima vya uzalishaji mbegu bora na kuwasimamia ili kuleta tija ya kilimo jambo litakalotoa hamasa kwa vijanawengi kujikita kwenye shughuli za kilimo kutokana na fursa za kipato pamoja na mnyororo wa thamani kwenye kilimo.

Mmoja wa vijana walioshiriki mafunzo hayo Besti  Alphonce Lihaya mkazi wa Luchingu Newala ambaye ni mfanya biashara ameishukuru Halmashauri kwa kuwa amenufaika sana na uwezeshaji uliofanyika hasa katika namna ya kujikita kwenye kilimo biashara nakubadilisha mawazo ya vijana kuhusu ajira na maisha halisi.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa