• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

WADAU WA ELIMU WATAKA USHIRIKIANO ILI KUINUA KIWANGO CHA ELIMU

Posted on: August 27th, 2025

Wadau wa elimu halmashauri ya Mji Newala wameomba uwepo wa ushirikiano baina yao, wazazi, wataalam wa elimu pamoja na wanafunzi utakaosaidia kuinua kiwango cha elimu.

Wameyaeleza hayo katika kilele cha maadhimisho ya juma la elimu ambapo wameitaka jamii kushiriki kwa vitendo katika kufundisha kwa njia ya malezi, kuchangia chakula cha wanafunzi, kuchangia mfuko wa elimu pamoja na kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi.

Kwa upande wake mwakilisha wa wenyeviti wa kamati za shule Bi. Mwanahamisi Songa amekiri kuwa wazazi wapo nyuma katika kusaidia ukuaji wa elimu “mimi naamini watataalam kazi yao wanafanya vizuri shida ipo kwetu sisi wazazi hatuoneshi ushirikiano watoto wanatupwa hovyo”.

Mwalimu Ibrahimu Adamu wa shule ya Msingi Makonga ameongeza kuwa wazazi wanashindwa kufuatilia mwenendo wa elimu ya watoto wao “ningeomba viongozi wale wazazi kule nyumbani tuwape semina kwamba mtoto akirudi shuleni basi yeye kazi yake ni nyumbani”.

Naye Mwalimu kiongozi wa kutoka shule ya msingi Makote, Mwl. Nunu Kupela ameomba ogezeko la walimu wa muda kupitia fedha za mfuko wa elimu ambapo ameeleza kuwa pamoja na mfuko huo kufanya vizuri katika miundombinu kwasasa iangalie suala la kuongeza walimu wa muda.

Aidha afisa mwakilishi wa jeshi la polisi wilayani Newala Derick Lekayo ameitaka jamii kuwapunguzia watoto muda wa kushiriki mambo ya kitamaduni hasa ngoma za unyango na mikesha ya sherehe.

“Kuna ngoma za kitamaduni tilizonazo katika wilaya yetu, ngoma hizo zina madhara makubwa sana kwenye maendeleo ya elimu, hizo ngoma ni nzuri ziendelezwe kwasababu ni utamaduni wa watu lakini ziwe na mda rafiki kwa watoto”

Hata hiyo Mwenyekiti wa shule ya msingi Nangwanda iliyopo kata ya Mcholi I Ndg. Abillah Mniha ameshauri, idara ya elimu ifanye mgawanyo wa walimu kwa uwiano wa wanafunzi katika shule ili kusaidia kupunguza changamoto ya uhaba wa walimu.

Katika taarifa ya ulaji wa chakula shuleni imeonyesha asilimia 85 pekee ya wanafunzi wa shule za msingi ndio wanaopata chakula shuleni na upande wa sekondari shule zote zinatoa chakula lakini si wanafunzi wote wanaokula kutokana na wazazi wao kutochangia.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WADAU WA ELIMU WATAKA USHIRIKIANO ILI KUINUA KIWANGO CHA ELIMU

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI CHANJO KWA MIFUNGO NG'OMBE 111 MBUZI NA KONDOO 1556 WAMESHAPATIWA CHANJO YA RUZUKU

    August 26, 2025
  • JESHI LA MAGEREZA NEWALA WACHANGIA DAMU, KUFARIJI WAGONJWA NA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA WILAYA NEWALA

    August 24, 2025
  • MHE. KUNDYA AWAAGIZA WATAALAM WA KILIMO NA FEDHA KUWAELISHA WAKULIMA KUHUSU UTUNZAJI WA FEDHA

    August 20, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa