• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wakulima wa alizeti wameishukuru Halmashauri ya Mji Newala Kwa uwezeshaji

Posted on: April 21st, 2023

Wakulima wa Alizeti wameishukuru Halmashauri ya Mji Newala kwa jitaihada zake za kuwasaidia kupata elimu na ushauri wa kukuza kilimo cha zao hilo mbadala katika kukabiliana na changamoto ya kiuchumi kwenye kilimo.

Bwana Hamadi Kadembe ambaye ni mkulima wa zao hilo amesema haikuwa rahisi kwake kuanza kulima zao hilo, lakini anaishukuru idara ya kilimo Halmashauri ya Mji Newala kupitia wataalam wake wamewajengea uwezo na kuwapa mafunzo katika hatua za kufikia uzalishaji wenye tija.

Kadembe amesema huu ni mwaka wake wa tatu tangu ameanza kulima alizeti na ameweza kukabiliana na changamoto za kimaisha kwa kuwa kilimo hicho kinampatia kipato tofauti na mtazamo wa wengi wanaodhani kulima zao hilo ni kupoteza muda kwa kuwa halina faida.

“Nimekua nikifuata kanuni na maelekezo ya maafisa kilimo wa Halmashauri ya Mji, huwa wanakuja kunitembelea na kuona tunalimaje, kasha wananishauri nifanye nini, kwa kweli wananitia moyo sana, mwanzoni nilikua nifeli kwenye korosho ndio basi lakini sasa nauza mafuta ya alizeti, napata kipato naendesha  maisha ya familia yangu vizuri.” Alieleza Mkulima huyo.

Kwa upande wake Bi. Mariam Machemba mkulima wa mazao mchanganyiko anasema analima zao la Alizeti kwa ajili ya matumizi ya nyumbani pamoja na biashara kutokana na maarifa aliyopata kutoka kwa wataalam wa kilimo na kwasasa anazalisha mafuta kiasi cha kuwauzia wafanya biashara wengine.

Aidha Bi. Machemba amewataka wanawake kubadili mitazamo yao na kuchangamkia kilimo hicho kwa kuwa kinamuwezesha kulipia mahitaji ya watoto shuleni, kumpatia mahitaji ya nyumbani pamoja na mahitaji binafsi.

Hata hivyo ameleeza kuwa changamoto za kulima Alizeti kulinganisha na mazao mengine na jambo kubwa ni kujua muda sahihi wa kupanda mbegu na hiyo inatokana na upya wa zao lenyewe. “wakati mwingine nashindwa kupata mazao yakutosha kutona na kuwahi au kuchelewa kupanda sehemu hiyo bado sijajua vizuri japo maafisa kilimo wananitembelea mara kwa mara shambani kwangu”.

Bwana Calistus Komba amesema kilimo cha Alizeti ni mpango wa Halmashauri kuhamasisha wananchi kulima mazao mbadala na kitu cha kufurahisha kuona mwitikio unaridhisha kila mwaka uzalishaji unaongezeka na wakulima wanaongezeka japo lengo kusudiwa bado halijafikiwa.

Aidha amesema halmashauri pamoja na kuhamasisha kupitia maafisa ugani lakini pia inawezesha katika ununuzi wa mbegu bora, kutambua maeneo yanayofaa kwa kilimo hizo pamoja na kununua mashine za kukamulia ambazo zinakabidhiwa kwenye vikundi vya wakulima wenyewe wazisimamie.

Halmashauri ya Mji Newala ni moja ya halmashauri ambazo zimekuwa kwenye jitihada kubwa ya kuinua uchumi kupitia kilimo cha mazao mbadala nje ya zao mama la Korosho kwa kuwekeza katika mazao ya Alizeti, Mpunga, Ufuta na Muhongo.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa