• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wananchi Newala kujiandaa na zoezi la sensa ya watu na makazi kwa kuwa na taarifa sahihi za kaya zao

Posted on: May 19th, 2022

Mkuu wa wilaya Newala  Mh. Mwangi Rajabu Kundya amewataka wananchi kujiandaa na zoezi la sensa ya watu na makazi 2022 kwa kuwa na taarifa sahihi za kaya zao kabla ya zoezi zipatikane takwimu za kweli.

Ameyazungumza hayo jana 18/05/2022 katika kikao cha kamati ya sensa ya wialaya cha utoaji elimu kwa maafisa watendaji wa kata wa halmashauri ya mji Newala kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Mhe. Kundya amewasisitiza watendaji wa kata kutoa elimu kwa wakuu wa kaya na familia kuwa na taarifa sahihi za watu wao ili kurahisha zoezi la sensa, jambo ambalo litapelekea kutimiza lengo mahususi la serikali la kupanga mipango ya maendeleo kwa wananchi wake.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya amewataka watendaji wa kata kushirikiana na madiwani katika kutoa elimu huku akiwaomba kubainisha changamoto na viashiria vyote vinavyoweza kujitokeza na kuathiri zoezi hilo ili kamati ya wilaya iweze kuzipatia ufumbuzi mapema.

Naye mratibu wa sensa halmshauri ya mji Newala Ndg. Simplis Frank amesema ili zoezi la sensa lifanikiwe ni lazima wananchi wapate uelewa wakutosha juu ya umuhimu wa kushiriki kuhesabiwa pamoja na manufaa yatokananyo na zoezi hilo.

Aidha amebainisha kuwa kamati ya maandalizi ya sensa ya wilaya imeazimia elimu ya sensa kuwa ajenda ya kudumu kwenye vikao vyote vya kiserikali kuanzia ngazi ya mtaa, kijiji, kata, halmashauri hadi wilaya kwa lengo la kujenga uelewa wa kutosha kwa wananchi.

Akiongea kwa niaba ya madiwani Mwenyekiti wa halmashauri hiyo ambaeni ni diwani wa kata ya Nanguruwe Mhe. Yusuph Kateule amesema wao kama madiwani watasimama mstari wa mbele katika kuwafikia wananchi kuwapa elimu jambo la msingi kwao ni kujengewa uelewa wakutosha.

Zoezi la sensa ya watu na makazi nchini linatarajia kufanyika mwezi wa nane kwa wananchi wote kuhesabiwa kila mmoja pale alipolala kuankia siku ya sensa Tarehe 23/08/2022.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa