• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wananchi Newala watakiwa kujihusisha na kilimo cha mazao mchanganyiko

Posted on: July 15th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini Mhe. George Mkuchika ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Maalum amewataka wananchi wa Newala kujihusisha na kilimo cha mazao mchanganyiko na kuacha kutegemea zao la korosho pekee.

Mheshimiwa Mkuchika ameyasema hayo Ijumaa July 14, 2023 akiwa kwenye siku ya pili ya ziara yake ya kijimbo ya kuongea na wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya serikali pamoja na kutoa ufafanuzi wa changamoto zinawakabili.

Amesema ni muhimu wakulima kuchukua hatua hiyo mambo yanabadilika na hata kwa msimu uliopita zao la korosho halikufanya vizuri. “Wapiga kura wangu wa Newala tusitegemee kilimo cha korosho peke yake mwaka jana msimu ulikua mbaya kwa korosho hatujui ni hali ya hewa.. hatujui tu, sasa basi una shamba la mkorosho lima na mbaazi, lima na mahidi ya kula”. Alisisitiza Mbenge huyo.

Aidha Mhe. Mkuchika amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kwapatia wakulima wa korosho pembejeo za bure huku akiwahimiza wakulima hao kuongeza jitihada katika uzalishaji kwa kuwa serikali imedhamiria kuliongezea thamani zao hilo kwa kuacha kuuza korosho ghafi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Yusuph Kateule amewataka wananchi kuchangia ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kulipa ushuru na tozo halali zilizoidhinishwa kisheria kwa kuwa ndizo chachu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya halmashauri.

Mwenyekiti Kateule amefafanua kwa mwaka wa fedha uliopita 2022/2023 malengo ya ukusanyaji mapato ya ndani hayakufikiwa kutokana na kuyumba kwa zao la korosho, baadhi ya wakulima kuuza mazao yao nje ya halmashauri pamoja na wafanyabiashara hasa wadogo kukwepa kulipa ushuru.

“Ndugu zangu jambo hili linatukwamisha sana kutekelezea mipango yetu ya maendeleo, tunashindwa kukamilisha miradi hivyo tunapokwepa kulipa ushuru sisi wenyewe ndio tunaathirika, hakikisheni unauza katika utaratibu uliowekwa katika kijiji chako”.  Alifafanua Mhe. Kateule

Afisa Mipango wa Halmashauri ya Mji Newala Bi. Sophia Makungu amewahimiza wananchi kujiandaa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya mwaka wa fedha 2023/2024 kwa sehemu ya mchango wa jamii hivyo vijiji vyenye miradi kupitia wananchi waanze kukusanya mchanga, kusafisha maeneo na maandalizi mengine yanayohitajika.

Hii ni siku ya pili ya ziara ya Mbunge wa Jimbo la Newala Mjini Mheshimiwa George Mkuchika ambayo atafanya mikutano, kukagua shughuli na miradi ya maendeleo katika kata zote 16 za jimbo hili ambapo leo ametembelea Kata ya Namiyonga na Kata ya Makote.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa