• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Wasimamizi wa Elimu wameshauriwa kuingia darasani ili kuisaidia jamii sawa na taaluma yao

Posted on: July 15th, 2022

Wasimamizi wa Elimu wa Halmashauri ya Mji Newala wameshauriwa kuingia darasani kufundisha masomo mbalimbali kulingana na ujuzi walionao ili kuisaidia jamii sawa na taaluma yao ya ualimu na kuacha kukaa ofisini pekee.

Wito huo umetolewa leo Ijumaa Julai 15, 2022 na Mthibiti Mkuu wa ubora wa shule wa Halmshauri ya Mji Newala Mwl. Hamisi Mbinga katika kikao cha wasimamizi wa elimu ngazi ya halmashauri cha kujadili namna ya kutekeleza maazimio yaliyotolewa na wasimamizi wa elimu ngazi ya Taifa mkoani Tabora.

Mbinga ameeleza kuwa kuanzia ngazi ya shule mpaka wizara wasimamizi wote wa elimu ni walimu, nafasi zingine walizo nazo ni ziada na wakati wowote wanaweza kuondoka na kurudi kufundisha hivyo si vibaya kwao kuendeleza umahiri wa taaluma yao kwa kutenga muda wa kufundisha darasani.

Aidha Mbinga amesema moja ya azimio lililowekwa katika kikao cha Taifa ni kuondoa ziro kwa sekondari mkakati ambao Mkoa wa Mtwara tayari ulishauweka katika mpango wake wa kuinua elimu, hivyo wasimamizi wakiwa mstari wa mbele kuweka msisitizo na kujitoa kwa vitendo itakua ni rahisi azimio hilo kufikiwa.

Mthibiti huyo ameongeza kuwa suala la nidhamu ni jambo lingine la muhimu la kuwezesha kupata matokeo chanya kwa kuanzia waalimu wenyewe na kama walimu wakikaa vizuri katika fundisha na kuhakikisha wanafunzi wanajua kusoma, kuhesabu na kuandika (KKK) ambapo mkoa umeweka kipaumbele eneo hilo na linahitaji nguvu ya pamoja.

Katika hatua nyingine Mbinga amesema ofisi yake ilibaini maeneo ambayo walimu wana changamoto ya kufikia ufundishaji wa kkk wameshatoa mafunzo kwa walimu na sasa halmashauri imepata mradi wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini (MEWAKA) mpango amabao unatarajia kutoa matokeo chanya ya ufundishaji na kuondoa tatizo la KKK ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.

Akizungumza kwa niaba ya wasimamizi wa elimu Mkuu wa idara ya elimu sekondari wa Halmashauri hiyo Mwl. Athuman Salum amesema wamepokea maazimio hayo kwa mtazamo chanya na kwa idara ya elimu sekondari imeongezewa nguvu katika mikakati yake yakuimarisha elimu hasa kwenye eneo la kuongeza ufaulu wa kidato cha tano na sita kwa daraja la kwanza na pili pamoja na kuondoa ziro kwa kidato cha nne.

Hata hivyo amepongeza mkakati huo wa elimu kitaifa na kuwataka wasimamizi wa elimu kuzingatia maazimio yaliyotolewa ikiwa pamoja na kuwajibika moja kwa moja katika kuingia darasani kufundisha hiyo itasaidia kuinua hari kwa walimu shuleni kutoa huduma bora za elimu.

 

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa