• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Ahadi ya Rais Dkt. Maguful ujenzi wa barabara ya Mnivata, Newala mpaka Masasi mbioni kukamilika

Posted on: May 22nd, 2020

Ahadi ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Maguful ya ujenzi wa barabara ya Mnivata, Nanyamba, Tandahimba, Newala mpaka Masasi wenye urefu wa kilometa 160 pamoja na daraja la Mwiti mkoani Mtwara, ipo mbioni kutekelezwa huku wananchi wakitakiwa kutumia fursa za ajira zitakazo jitokeza.

Hayo yameelezwa mjini Newala Jumatano Mei 20, 2020 na Ofisa Sayansi ya Jamii Mkuu wa wakala wa barabara Nchini (TANROADS) makao makuu ndg. Gibson Mwaya, wakati wa kikao cha Tanroads na madiwani, wakuu wa taasisi, watendaji wa Kata pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya mji Newala, cha kuelezea hatua za utekelezaji wa mradi huo.

Mwaya amesema uzoefu unaonyesha wananchi  waliopo kwenye maeneo ambayo miradi ya maendeleo inatekelezwa hawajitokezi kwenye kuomba kazi hata sizizo na taaluma maalum, badala huwapisha wageni kutumia fursa hiyo na wao kuwa watazaji hivyo amewataka wawakilishi hao kuwaelimisha wananchi kuwa hiyo ni fursa ya ajira na maendeleo.

Aidha amewaka wananchi kutambua kuwa maendeleo yoyote yana hasara  ndani yake hivyo amewataka kuwa makini na muingiliano na wageni watakao kuja wakati wa utekelezaji hasa katika kujikinga magonjwa ya maambukizi ya zinaa kama UKIMWI, mimba zisizotarajiwa, uvunjivu wa ndoa pamoja na mambo mengine ya anasa na starehe.

Aidha amempongeza Mhe. Rais kwa kutafuta vyanzo mbalimbali vya fedha na Bank ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) imeonyesha nia ya kuufadhili mradi huo, na sasa wapo kwenye hatua za mwisho za mapitio ili kutoa fedha za utekelezaji, na hiyo ni hatua ya utekezaji wa ahadi yake aliyowaahidi wananchi mwaka jana akiwa kwenye ziara yake mkoani Mtwara.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya mji Newala ndg. Adrew Mgaya amempongeza Mhe. Rais kwa ahadi zake za kweli zinazotekelezeka, huku akieleza kuwa utekelezaji wa mradi huo ni hatua kubwa ya kuinua uchumi wa Taifa na wananchi wa kawaida, hivyo halmashauri imejipanga kutumia fursa hiyo kuongeza pato kwa kuboresha miundombinu yake ya makusanyo.

Kikao hicho kimefanyika jana Jumatano tarehe 20/05/2020 katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya mji newala ambapo awali Tanroads ilipanga kufanya vikao kwenye vijiji vinavyopita mradi huo kuongea na wananchi kuwaeleza mambo mbalimbali ikiwemo fidia, faida na athari za mazingira zinazoweza kujitokeza lakini kutokana na uwepo wa ugonjwa corona wameamua kuongea na wawakilishi wa wananchi ili kupunguza hatari ya maambukizi.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa