• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

Posted on: August 4th, 2023

Halmashauri ya Mji Newala imeidhinishiwa shilingi Bilioni 21.5 kuwa bajeti yake ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 20223/2024 huku Mkuu wa wilaya ya Newala Alhaj. Mwangi Rajabu Kundya akiitaka halmashauri hiyo kutumia fedha za miradi ya maendeleo kwa kuzingatia malengo ya Taifa.

Alhaj. Kundya ameyasema hayo katika mkutano wa baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo wa robo ya nne 2022/2023 uliofanyika Agosti 03, 2023 na kuhimiza uadilifu katika usimamizi ili kupata matokeo bora yakujivunia kwa kuwa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka serikali kuu ni fursa.

Aidha ameeleza kuwa hali ya utekelezaji wa miradi ni ya wastani hivyo uadilifu na uaminifu uongezeke ili ikamilike kwa wakati na katika ubora, “ndugu zangu kupata miradi ni fursa.. fursa muhimu sana… fursa ambayo huko nyuma ilikua inapatikana kwa bahati nasibu… tuzitumie fursa hizi”. Alilisitiza Kundya.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya amewataka waheshimiwa madiwani kuweka kipaumbele katika usimamizi utakaosaidia kubaini mapungufu kwa kuwa hilo ni jukumu lao la kusimamia maendeleo ya halmashauri na sio kuwaachia wataalam peke yao ambao baadhi yao wameonekena kutokuwa waadilifu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Yusuph Kateule amewaangiza madiwani  kushirikiana na watendaji wengine wa halmashauri kuhakikisha kila chanzo cha mapato kilichoainishwa kwenye mpango wa bajeti kinakusanywa kikamilifu katika maeneo yao.

Aidha Mhe. Kateule ameonya matumizi mabaya ya fedha za serikali kwa wataalam na kuwataka kufanya matumizi kwa mujibu wa mpango wa bajeti na vipaumbele vyake vinavyolenga kutoa majibu ya maendeleo kwa wananchi wa halmashauri hiyo.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndg. Geofrey Nnauye ameomba ushirikiano na umoja pamoja na kumtanguliza Mungu toka kwa wasimamizi, madiwani na wataalum kwa kuwa hiyo ndio njia pekee ya kufikia mafanikio katika kuwatumika wananchi.

“Ndugu zangu tukimtanguliza Mungu mbele nina imani kabisa tutavuka salama, na lengo lile la kuwatumikia wananchi wetu tutalitimiza kwa madhumuni hayo amabayo tutakuwa tumeyaweka”. Alieleza Mkurugenzi huyo.

Bi. Sophia Makungu Afisa Miapango wa Halmashauri hiyo  katika mkutano huo ameainisha mchanganuo wa bajeti  hiyo kuwa, shilingi bilioni 11.9 ni mishahara na matumizi mengine ya ofisi, Ruzuku ya mairadi ya maendeleo kutoka serikali kuu ni shilingi bilioni  3.9.

Shilingi bilioni 2.6 fedha kutoka kwa wahisani, Makusanyo ya mapato ya ndani shilingi bilioni 2.6 pamoja na mchango wa jamii shilingi milioni 280 unaotokana na shughuli za kujitolea nguvu kazi wakati wa kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa