• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Fedha za mfuko wa elimu shilingi milioni 155 zatekeleza miradi ya elimu Newala Mji

Posted on: July 31st, 2025

Bodi ya mfuko wa elimu halmashauri ya Mji Newala na kamati tendaji ya mfuko imefanya ziara ya kukagua miradi iyopewa fedha na mfuko huo zaidi ya shilingi milioni 155 na kuridhishwa na matumizi yake.

Mara baada ya ziara Mwenyekiti wa bodi hiyo Ndg. Jarome Linyembe amempongeza mkurugenzi wa halmashauri na watendaji wake kwa usimamizi nzuri wa matumizi fedha katika miradi ya elimu msingi na sekondari.

“Kwa kweli hali ya miradi inaonekana ni mizuri hata kwa kuiangalia hii inaonesha usimamizi wake ni nzuri tunampongeza sana mkurugenzi wa Mji Newala kwa kukubali kusikiliza maoni ya bodi na kusimamia utekelezaji wake.” ameeleza Linyembe.

Hata hivyo mwenyekiti huyo ametaka shughuli zote zinazotekelezwa na mfuko huo zifahamike kwa wananchi “fedha hizi ni michango ya wakulima na wananchi wa halmashauri hii kupitia mauzo ya mazao yao yanayouzwa kwa stakabadhi ghalani ikiwemo korosho, mbaazi na ufuta.”

Aidha Linyembe amesema lengo la mfuko huo ni kusaidia maendeleo ya elimu katika kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji, kutoa motisha pamoja na miundombinu ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha sekta ya elimu nchini.

Mkuu wa idara ya elimu sekondari Mwl. Diana Sonno amesema mfuko huo kwasasa umekuwa chachu ya kusaidia ukamilishaji wa madarasa, maabara pamoja na posho kwa walimu wa muda nah atua hiyo inapelekea kupunguza ukubwa wa changamoto zinazoikabili idara ya elimu kwa ujumla.

“Ndugu mwenyekiti wa bodi, tunashukuru sana uwepo wa mfuko huu yaani umekua msaada sana kwetu sisi watu wa elimu hasa idara yetu mumetupata fedha shilingi milioni 5 za kukamiliza madarsa 5, shilingi milioni 45 kukamilisha maabara 3, mumetoa shilingi milioni 50.15 kununulia viti 250 na meza 250 pamoja na madawati 250” Amefafanua.

Kwa upande wake mratibu wa mfuko huo Mwl. Innocent Kerenge amewashukuru wananchi kwa michango yao huku akifurahishwa na awamu ya kwanza ya utekelezaji kwa kupunguza changamoto ya kukosekana maabara katika shule za sekondari.

“kwa kweli nimefurahi sana mwaka jana hali ilikuwa mbaya hapa Sekondari ya Dr. Alex wakati wa mtihani wa taifa tulikuwa na maabara moja kwa masomo ya sayansi lakini kukamilika kwa hii nyingine itaondoa ile hali ya wasiwasi wakati wa mitihani kwamba itakuwaje?” Ameeleza Mwl. Kerenge.

Aidha pia miradi mingine iliyopewa fedha ni ujenzi wa chumba cha darasa shule ya msingi Mnanje shilingi milioni 20, madarasa mawili shule ya msingi Mpilipili shilingi milioni 40 pamoja na shilingi milioni 15 za kuchangia ujenzi wa nyumba ya mtumishi shule ya msingi Nambunga.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Fedha za mfuko wa elimu shilingi milioni 155 zatekeleza miradi ya elimu Newala Mji

    July 31, 2025
  • WALIMU KIDATO CHA SITA WAPONGEZWA KWA MATOKEO MAZURI

    July 30, 2025
  • Mkurugenzi Nnauye amewapongeza wataam wa afya na watendaji wa kata utekelezaji mkataba wa lishe

    July 30, 2025
  • WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    July 02, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa