• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

HALI YA AFYA NA LISE YA WATOTO NEWALA MJI YAENDELEA KUIMARIKA

Posted on: August 7th, 2025

Hali ya afya na lishe ya watoto ndani ya halmashauri ya Mji Newala imeendelea kuimarika kutokana na jamii kupata uelewa pamoja na kujitokeza kushiriki katika masuala yanayohusu lishe.

Hayo yamebainishwa na afisa lishe wa halmashauri hiyo Bi. Beatrice Saria katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama duniani katika zahanati ya Tupendane iliyopo kata ya Tulindane ambapo amesema inatokana na jamii kujihusisha moja kwa moja katika lishe.

“wazazi wameweza kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho tunayoyafanya kila robo, katika shughuli zetu za kila siku na elimu tunazotoa kupitia mikutano ya kijiji, kwa njia ya redio kwahiyo tunaona kuna mabadiliko makubwa na kuna tofauti ya mwanzo na sasa.”

Aidha ameeleza kuwa katika maadhimisho hayo wazazi 2550 wamepata elimu ya unyonyeshaji maziwa ya mama, watoto 1750 wamefanyiwa tathmini ya hali ya lishe na 14 kati yao saw ana 0.8% ndio waliokutwa na ukondefu pamoja na wazazi 980 wenye watoto wa miezi 0-23 wamepatiwa unasihi wa ulishaji watoto wadogo na wachanga.

Ndugu Chibwana Fadhili kutoka kitongoji cha Mfalanyaki mzazi aliyemleta mtoto wake kupimwa hali ya lishe na kupata elimu amesema malezi ya mtoto yanawahusu wazazi wote hivyo yeye kama baba anawajibu wa kusimamila jukumu hilo.

Bi. Fadhila Musa mkazi wa Mnuwi amesema maadhimisho yamempa faida kubwa ikiwemo kupata elimu ya unyonyesha huku akiiomba jamii kushirikiana katika malezi ya mtoto kwa kuwa malezi bora yanaleta ukuaji bora.

Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji maziwa ya mama duniani yalianzia agosti 1-7, 2025 yakiwa yamebeba kauli mbiu isemayo “Thamini Unyonyeshaji: Weka Mazingira Wezeshi Kwa Mama Na Mtoto.”

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. KUNDYA AWAAGIZA WATAALAM WA KILIMO NA FEDHA KUWAELISHA WAKULIMA KUHUSU UTUNZAJI WA FEDHA

    August 20, 2025
  • TAASISI NA VITENGO VINAVYOSIMAMIA USAFI MSHIRIKIANE KUTOA ELIMU KWA JAMII

    August 19, 2025
  • MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UTAMBUZI WA WANYAMA

    August 16, 2025
  • JAMII YATAKIWA KUWAAMINI VIJANA NA KUWAPATIA FURSA

    August 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa