• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Mji Newala kinara kwa kufaulisha darasa la 7 mwaka 2019 mkoani Mtwara,

Posted on: October 22nd, 2019

Halmashauri ya Mji Newala imeibuka kuwa kinara kwa kufaulisha wanafunzi walifanya mtihani wa matokeo ya darasa la 7 mwaka 2019 mkoani Mtwara, katika matokeo yalitangazwa hivi karibuni tarehe 15/10/2019 na baraza la Mitihani nchini NECTA.

Katika matokeo hayo halmashauri ya mji Newala yenye shule za msingi 45, imeshika nafasi ya 12 kitaifa sawa na ufaulu wa asilimia 94.04 kwa wanafunzi wote 1,896 waliofanya mtihani huo, wavulana 898 na wasichana 998, ambapo kati yao wavulana 852 wamefaulu na wasichana 931.

Ofisa Elimu Msingi wa halamsahauri hiyo Mwl. Mohamed Mwende amesema, mafanikiwa hayo hayakuja kwa bahati mbaya bali ni jitihata na mipango ya pamoja baina ya ofisi yake, waalimu, wazazi, pamoja na wanafunzi wenyewe kuzingatia walichofundishwa darasani.

Hata hivyo amefafanua kuwa, wanajivunia mafanikio hayo kwa kuwa tangu mwaka 2016 ufaulu umekua unapanda kwani 2016 ufaulu ulikua 60% nafasi ya 5 kimkoa na 145 nafasi ya kitaifa,  mwaka 2017 ufaulu ulikua 72% nafasi ya 3 kimkoa na 90 nafasi ya kitaifa,  mwaka 2018 ufaulu ulikua  91.5% nafasi ya 1 kimkoa na 12 nafasi ya kitaifa  sawa na mwaka huu 2019 huku ufaulu ukifikia 94.04%.

Aidha ameeleza kuwa agizo alilolitoa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa mapema mwaka jana 2018 la kuzitaka shule zote mkoani humo kuhakikisha zinamaliza kufundisha mtaala mwezi juni, limesaidia kuwaanda wanafunzi vizuri, kwa kubaini mapungufu mapema na kuyafanyia kazi kabla ya mtihani.

Sambamba na hilo Mwl. Mwende amewataka wazazi kuhakikisha wanawandaa mapema watoto wao na masomo ya sekondari, na hiyo ndiyo fahari pekee na matunda ya kazi waliyoifanya na kwa namna yoyote ile waepuke kuwawekea vikwazo vya kutowaendeleza kimasomo kwa kuwaozesha au kutogharamia mahitaji yao ya shule.

Katika hatua nyingine amewataka wazazi wenye watoto wa umri wa miaka 4-5, kwenda kuwaandikisha kwenye madarasa ya awali kwani baada ya miaka miwili watoto wataoandikishwa darasa la kwanza ni wale waliopo kwenye madarasa hayo tu, kwani wao ndio watakua wameandaliwa kwa ajili ya kupata elimu ya msingi.



 

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa