• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Mji Newala yamwagiwa sifa kwa kuongoza kufaulisha darasa la saba 2018

Posted on: December 14th, 2018

 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Gaspar Byakanwa, leo Ijumaa December 14, 2018 ametoa pongezi kwa halmashauri ya Mji Newala, kwa kushika nafasi ya kwanza kimkoa katika ufaulu wa wananfunzi wa darasa la saba mwaka huu.

Mkuu wa mkoa ametoa pongezi hizo kwenye kikao cha pamoja kati yake na wakuu wa wilaya, makatibu tawala, wakurugenzi wa halashauri, wenyeviti wa halmashauri na maafisa elimu wa mkoani hapa, kikao kilichofanyika mjini Newala kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Newala.

Hata hivyo Byakanwa amesema japokuwa mkoa kwa ujumla umejitahidi kutimiza malengo yake ya kitaifa ya kufaulisha wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza 2019, kwa kushika nafasi ya 8, kutoka nafasi ya 26 mwaka jana 2017 bado halmashauri ya Mji Newala ni ya mfano kwani imetekeleza makubaliano.

Aidha Mkuu wa mkoa ameitaka halmashauri ya Mji kutobweteka na matokeo hayo badala yake iongeze juhudi ili kuendelea kutetea nafasi hiyo huku akiutaka mkoa kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha elimu na kufikia lengo ya kufaulisha kwa asilimia 100 pamoja na kuwa kwenye nafasi 3 za juu za ufaulu kitaifa.

Katika hatua nyingine Mkuu wa mkoa amempongeza Mkurugenzi wa Mji Newala Andrew Mgaya, kwa mikakati yake ya kukabiliana na changamoto kwenye sekta ya elimu hasa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa  na uhaba wa madawati kwani halamshauri hiyo haina upungufu wa madawati na ipo kwenye hatua za kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa utakaomaliza tatizo hilo kwa asilimia 100.

“sitaki kuona wanafunzi yoyote anasoma chini ya mti katika mkoa wangu haiwezekani, wakurugenzi hakikisheni hilo halijitokezi na mujadiliane na wabunge wenu fedha za mfuko wa jimbo kipaumbele chake kiwe ni kujenga vyumba vya madarasa na madawati na zoezi hilo ifikapo February 2018 liwe milikamilika, na ninawaagizeni wakuu wa wilaya simamieni kikamilifu zoezi hili katika wilaya zenu na lianze mara moja” amesisitiza Byakanwa

Awali akizungumza wakati anamkaribisha mkuu wa mkoa katika kikao hicho Afisa Elimu Mkoa wa Mtwara Bi. Germana Mung’aho amesema halmashauri ya Mji Newala imefaulisha kwa asilimia 91 na kushika nafasi ya kwanza kutoka nafasi ya 3 mwaka jana ambapo ilifaulisha kwa asilimia 72.

Mung’aho amefafanua kuwa jumla wa wanafunzi 20,100 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2019 mkoani hapa, na kati yao wasichana ni 10,943 na wavulana 9157 huku akieleza kuwa huo ni wastani wa mafanikio ya asilimia 100 na kuitaka jamii kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa wanajiunga na masoma na kumaliza.

Ufaulu wa darasa la saba kimkoa mwaka 2018 unaongozwa na 1. halmashauri ya Mji Newala, 2.halmashauri ya Mtwara Vijijini, 3.halmashauri ya Mji Masasi, 4.halmashauri ya Mji Nanyamba, 5.halmashauri ya Mtwara Manispaa, 6.halmashauri ya wilaya Newala, 7.halmashauri ya wilaya Tandahima, 8.halmashauri ya wilaya Masasi na iliyoshika mkia ni 9.halmashauri ya wilaya Nanyumbu

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa