• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

HALMASHAURI YA MJI NEWALA YAWEKA MKAKATI WA KILIMO CHA MAZAO YA BIASHARA

Posted on: August 9th, 2025

Halmashauri ya Mji Newala imeweka mkakati wa kuwafikia wakulima katika maeneo yao kuwahamasisha na kuwapa elimu ya kulima mazao ya biashara ili kuyafikia malengo yaliyowekwa na mkoa Mtwara.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndg. Geofrey Nnauye katika kilele maadhimisho ya sikukuu ya wakulima katika viwanja vya maonesho ya nanenane kanda ya kusini kwa kueleza kuwa halmashauri ipo katika kutekeleza mkakati wa kuinua uchumi kupitia mazao ya biashara.

“Na mkakati ambao tumeweka ndani ya mkoa ni kuinua uchumi wa wananchi kupitia kilimo hasa mazao ya biashara na sisi wananchi wetu wa halamshauri ya Mji Newala ni wakulima na tumetengeneza mkakati wakupita kwenye vijiji vyetu kuhamasisha wananchi walime mazao ya kibiashara”.

Kwa upande wake afisa kilimo wa halmashauri hiyo Ndg. Calistus Komba amesema katika maonesho ya mwaka 2025 walijikita katika utoaji elimu kupitia vitalu vya mashamba darasa hasa kwa mazao ya ufuta, alizeti, mpunga, karanga na mazo mengine ya chakula.

Komba ameeleza kuwa “Wananchi wamejifunza kwakweli tunaamini mwaka huu tutakuwa na mafanikio makubwa zaidi ya mwaka jana na pia wataenda kufanya shughuli za kilimo kwa tija, kwa maana ya kuongeza kipato kwa mtu mmoja mmoja na serikali nayo itaongeza pato”. 

Katika hatua nyingine amewataka maafisa ugani wanapotemebea maonesho hayo kutembelea maeneo mengine kwenda kujifunza mbinu na teknolojia mpya ili wakatumie katika shughuli zao za kuwahudumia wakulima.

Afisa kilimo anayeratibu maonesho ya nanenane halmashauri ya Mji Newala Bw. Juma Kahamba amefahamisha kuwa elimu waliyoitoa kwa wakulima wakiizingatia inatosha kuwapatia mafanikio makubwa katika shughuli zao.

Hata hivyo mratibu huyo amewaomba wakulima kuunga mkono juhudi za halmashauri katika kulima mazao tofauti tofauti ya biashara kwa kuwa yanafaida za kiuchumi ambazo hazitegemei mapato ya msimu mmoja.

Halmashauri ya Mji ya Newala pamoja na kutoa elimu ya kilimo bora katika maonesho hayo lakini pia imetoa elimu ya ufugaji, uchaguzi, usaidizi wa kisheria pamoja na kuonesha bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wajasiriamali wa halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. KUNDYA AWAAGIZA WATAALAM WA KILIMO NA FEDHA KUWAELISHA WAKULIMA KUHUSU UTUNZAJI WA FEDHA

    August 20, 2025
  • TAASISI NA VITENGO VINAVYOSIMAMIA USAFI MSHIRIKIANE KUTOA ELIMU KWA JAMII

    August 19, 2025
  • MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UTAMBUZI WA WANYAMA

    August 16, 2025
  • JAMII YATAKIWA KUWAAMINI VIJANA NA KUWAPATIA FURSA

    August 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa