• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

HALMASHAURI ZA WILAYA YA NEWALA MKOANI MTWARA ZATAKIWA KUTENGA BAJETI YA LISHE

Posted on: November 23rd, 2018

Halmashauri za Wilaya Newala Mkoani Mtwara, kupitia kamati zake za lishe, kwa pamoja zimetakiwa kutenga shilingi elfu moja kwa idadi ya watoto wenye umri  chini ya miaka mitano na kutekeleza kwa vitendo hatua za kuandaa bajeti endelevu, itakayo washirikisha wadau wengine wa lishe.

Rai hiyo imetolewa jana Alhamisi Novemba 22, 2018 na Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo, wakati anafungua Semina ya mpango wa uandaaji wa bajeti ya lishe 2019/2020 kwenye halmashauri, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya  Mkuu wa wilaya hiyo ambapo amesema hatua hiyo ni muhimu katika kukabiliana na Utapiamlo.

Mkuu wa Wilaya ya Newala akiongea na wajumbe wa Mafunzo ya Mpango wa kuandaa bajeti ya lishe kenye halmashauri 2o19/2020 wilayani Newala

Mkuu wa wilaya alisema “Ndugu washiriki, lishe duni ni chanzo kikuu cha upungufu wa damu kwa wajawazito ambao huwaongezea uwezekano wa kupoteza maisha wakati au baada ya kujifungua,  kwa upande wa watoto wachanga na wadogo, lishe bora katika siku elfu moja za mwanzo wa maisha yao, ni muhimu yaani tangu mimba kutungwa mpaka anapotiza miaka miwili ,ndio msingi thabiti wa ukuaji wa mwili na maendeleo yake ya kiakili katika kujifunza na uwezo mkubwa zaidi wa kujiingizia kipato.”

Kwa upande wake Mwezeshaji wa Masuala ya Mipango na Bajeti Kitaifa kutoka 0R-TAMISEMI, bwana Allan Bendera, amesema utekelezaji bajeti ya lishe ni mwitikio wa sera ya taifa kuhusu lishe hivyo ameziomba kamati kuwa na vikao kazi vya kujadili makubaliano sambamba na kupeleka elimu kwenye ngazi ya chini ya uongozi kuanzia mitaa, vijiji na kata.

Hata hivyo ameeleza kuwa halmashauri kutenga shilingi 1,000 kwenye bajeti ya lishe kwa kundi la watoto linatakiwa lipewe kipaumbele, “kwasasa masuala ya lishe yamepewa umuhimu pekee kwa kuangalia athari za kijamii na kiuchumi katika maeneo yetu tunayoishi, hivyo ni vema kujadili kwa kina ili kupata mipango mizuri, imara ambayo inaenda kuondoa matatizo ya Utapiamlo pamoja na Udumavu katika jamii.” alieleza Bendera.

Mwezeshaji wa Masuala ya Mipango na Bajeti Kitaifa kutoka 0R-TAMISEMI, bwana Allan Bendera.

Wenyeviti wa halmashauri hizo, Mheshimiwa Chitwanga Rashid Ndembo wa Wilaya na Mheshimiwa Abdul Katani Dudu, diwani wa Kata ya Julia aliyekaimu uwenyekiti halmashauri ya Mji wamesema watahakikisha mpango wa kutenga bajeti hiyo inafanikiwa japokuwa ipo changamoto ya vyanzo vya mapato.

Nao wajumbe wa semina hiyo wamesema, mafunzo hayo yamesaidia kutoa uelewa wa pamoja baina ya idara mbalimbali za halmashauri zinazohusika kuandaa bajeti hiyo, na kuahidi kuzingatia muongozo wake ili kufikia lengo kusudiwa serikali huku wakitoa pongezi kwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mtaa (OR-TAMISEMI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na  LisheTanzania na Wadau wa Maendeleo walioandaa Mafunzo hayo.





Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa