• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Hotuba ya Mhe. Rais Magufuli Wakati wa Kuwaapisha Mawaziri Leo Tarehe 12/11/2018 Ikulu DSM

Posted on: November 12th, 2018

Hotuba ya Mhe. Rais Magufuli Wakati wa Kuwaapisha mawaziri wapya leo tarehe 12/11/2018 Ikulu Dar es salaam


RAIS MAGUFULI: Kwa namna ya pekee niwapongeze waliokuwa Mawaziri wa Wizara ya Kilimo na Viwanda kwa kufika kwenu. Kuna gazeti linanikumbusha kuwa Mawaziri 20 nilioanza nao wamebaki 11 na 9 nimewatengua. Nimejiuliza miaka 2 iliyobaki wangapi watakuwepo?


RAIS MAGUFULI: Katika kazi hizi za kuleta maendeleo na kufikia malengo sio lazima wote mfike. Kuna mambo ambayo tulijiwekea malengo ya kuyafikia ikiwemo sekta ya Kilimo na Viwanda. Wizara hizi zinauwezo wa kutatua changamoto ya ajira


RAIS MAGUFULI: Sekta ya Kilimo na Viwanda ni sekta nyeti na mara nyingi nimekuwa nikigombana na Waziri Mkuu nikimuuliza mbona hiki hakiendi? Mara nyingine nampigia simu saa 8 usiku nikimtuma huku na huku kwasababu ndio kiranja wa Mawaziri


RAIS MAGUFULI: Nimekuwa nikiona Wizara zinazofanya kazi vizuri. Ukienda TAMISEMI kuna vijana wanafanya vizuri, Seleman Jaffo. Nimetoa mfano wa huyu kwasababu ndio kijana mdogo na nimesikia ana wake wanne


RAIS MAGUFULI: Limetokea suala la Kahawa nilimtuma Waziri Mkuu akaenda kulishughulikia. Tena wengine wanaovuka mpaka kwenda kuuza Kahawa wanatokea kwa Waziri Mwijage nikajiuliza au ameegemea kwenye Viwanda amesahau Biashara?


RAIS MAGUFULI: Kuna kiwanda kilikuwa kimekaa bila ya uzalishaji nikamtuma Waziri Mkuu akaenda kutatua Mpaka nikamwambia sasa nitakufanya uwe Waziri wa Viwanda au Kilimo


RAIS MAGUFULI: Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazozalisha Korosho kwa wingi Duniani. Tumebahatika kupata Bunge kama chombo cha kutunga sheria, taasisi na Bodi mbalimbali lakini linapokuja suala la mazao ya Watanzania siwaoni wakifanya juhudi


RAIS MAGUFULI: Mkurugenzi wa TANTRADE hajui kama anatakiwa kutafuta masoko ya mazao yetu au yeye anasubiri tarehe 1 mwezi wa 7 ili afungue maonesho ya saba saba. Mkurugenzi wa TANTRADE anasubiri kupokea viingilio vya maonesho ya saba saba


RAIS MAGUFULI: Kulikuwa na kikao kilichoitishwa na Waziri Mkuu na Mimi nikaona nivamie na Waziri Mkuu hakunifukuza nikafurahi. Niliyoyasikia humo yaliniumiza, Mwakilishi wa Bodi ya Korosho nilimuuliza bei ya Korosho akasema Tsh. 1,000 na Bei elekezi waliyoitoa ni 1,500


RAIS MAGUFULI: Niliangalia mataifa mengine nikaona bei ya Korosho imeshuka kidogo India. Nikaona Bodi ya Korosho haipo kwaajili ya manufaa ya Watanzania. Nikawapa bei elekezi ya Tsh. 3000 lakini siku ya mnada waliongeza shilingi 1 aliyeongeza zaidi alinunua kwa 3016


RAIS MAGUFULI: Nikagundua huu ni mchezo uliopangwa ili mvua ikianza wakainunue Korosho kwa bei ya chini kwasababu Wakulima wataogopa kuharibikiwa. Lakini kwenye hili sikuona statement ya Waziri wa Kilimo wala Viwanda


RAIS MAGUFULI: Nimeamua yafuatayo. Walioleta mapendekezo kwako achana nao watakuja kuleta masharti. Wanaoendelea kuja wala wasihangaike nimeshafunga. Korosho tunanunua wenyewe.


RAIS MAGUFULI: Nimepiga mahesabu ingawa Mimi si mchumi, ukibangua Korosho Kg 3 unapata Kg 1 ukichukua Tani laki 2 utapata Kg elfu 73 na ukigawa kwa Watanzania kila Mtu anapata Kg 2 na Korosho zitakuwa zimeisha


RAIS MAGUFULI: Ile Korosho tutainunua kwa Tsh. 3300 na kila Mkulima alipwe bila ya kukatwa hela yoyote. Maghala yote yalindwe na JWTZ na wameshakaa tayari kusimamia zoezi hili ili Korosho mbaya kutoka nchi jirani huwa inaletwa


RAIS MAGUFULI: Korosho nyingine itapelekwa kwenye Kiwanda kilichopo Lindi kilichorudishwa kwa Serikali juzi kinauwezo wa kubangua tani 73 elfu. Na kuanzia leo Kiwanda hiki nimelipa Jeshi na wao wakishindwa kikiendesha nitawapa wengine. Jeshi liende likakizingire


RAIS MAGUFULI: Korosho yetu ni daraja la kwanza duniani lakini Wananchi wanaishi maisha ya chini na mabodi yapo tu. Tunabaki kuwasikiliza matapeli wanaozungumza kwenye vyombo mbalimbali kwa faida zao na wanaowatuma


RAIS MAGUFULI: Niliowateuwa mkaanze kufanya kazi leo. Tatizo hamfanyi kazi kwa kushirikiana nendeni mkaanzishe ushirikiano. Benki ya Wakulima watatoa fedha na Jeshi litaichukua Korosho na hakuna itakayoibiwa Mimi nawajua. Jeshi likabangue kwa namna watayoona inafaa


RAIS MAGUFULI: Taasisi ya Uwekezaji ihamie kwa Waziri Mkuu na itakapokuwa chini ya Waziri Mkuu hata Mimi nitakuwa na uwezo wa kusimamia. Kuna wawekezaji wa ajabu wamekuja nchi hii. Mtu anakwambia anawekeza Bagamoyo lakini anakwambia usiwekeza hadi Pangani


RAIS MAGUFULI: Tusifikirie wawekezaji wanakuja kutusaidia. Kuna mambo ya ajabu kabisa tena mkataba unawapa kwa miaka 99. Tumekuwa na Bodi zisizofanya kazi.


RAIS MAGUFULI: Sitajali kubadilisha Mawaziri kila wakati hata kama watakuwa wanabadilishana kila baada ya miezi 5. Zao la Korosho limeingiliwa sana hata Wanasiasa walikuwa wanaweka watu wao na kufanya biashara ya 'Kagomba'. Na ndio wasemaji wakubwa wa watu wa huko


RAIS MAGUFULI: Nawapenda wote lakini kwenye ukweli lazima tuambiane. Benki Kuu mwende mkalisimamie hili kuna watu wanataka kuleta fedha za utakatishaji kwenye benki zetu. Wengine walitaka kuingiza Bilioni 150 kupitia benki flani kwahiyo Gavana endelea kubana hivyo hivyo


RAIS MAGUFULI: Unisamehe Jaffo nimekusifu hadharani na Utumishi nimeona nimuongezee Mzee wetu Mkuchika kwasababu alibaki peke yake hata Mtu wa kumtuma alikuwa anakosa. Jaji Mkuu nitakuletea majina ya Majaji wanaochukua rushwa


RAIS MAGUFULI: Jaji Msofe tumekuteua kwasababu umestaafu kwa rekodi nzuri. Pia Jaji Mkuu ninakushukuru kwa ushauri wako na nitakuletea majina ya wanaofanya vibaya. Mawaziri mlioteuliwa msidhani mtapendwa na baadhi ya Wabunge


RAIS MAGUFULI: Baada ya kutangaza mabadiliko Dkt. Tizeba alinipigia simu, nikajiuliza nipokee au nisipokee maana nisije nikaonge kitu watu wakazimia. Lakini alikuwa akinishukuru kwa kuhudumu kipindi chote bila ya kuishia jela


RAIS MAGUFULI: JWTZ nendeni mkafanye kazi hakuna mlilowahi kushindwa. Ukuta wa Mirelani mlijenga miezi 3 badala ya 6. Hii oparesheni ya Korosho haiwezi kuwashinda. Pangeni vikosi vya kubangua Korosho, tukikosa wanunuzi tutazila maana ni kilo 2 tu kwa kila Mtanzania


RAIS MAGUFULI: Wakulima wa Zabibu wanalalamika na Wizara ya Fedha, Viwanda na Kilimo zipo kwanini wanashindwa kutatua. Sio kila kitu mpaka Mimi niseme. Sasa hili la Zabibu mwende mkalimalize sio mpaka niseme mkalimalize


RAIS MAGUFULI: Hao wanaosema tunatumbua ni wachonganishi. Waziri Mkuu nenda ukasimamie hili bei ya Korosho ni Tsh. 3300 hata tukipata hasara potelea mbali. Kokoa kule Kyela mkaifuatilie kwasababu Wananchi wananiandikia 'vimeseji'


RAIS MAGUFULI: Makatibu Wakuu wa Wizara nilizozifanyia mabadiliko msifikirie nimewasahau au kwamba ninyi ndio mmetulia sana. Kuna mambo yanakwama kwasababu ya Makatibu Wakuu. Mwende Mkabadilike

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa