• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Jamii, Wadau, Mashirika na wasimamizi wa sheria wametakiwa kijikita katika kuzuia ndoa za utotoni

Posted on: March 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa Mtwara Kanali Abbas Ahmad Abbas ameitaka jamii, wadau, mashirika na wasimamizi wa sheria wajikite katika kuweka mipango ya kuzuia ndoa za utotoni na matukio ya vitendo vya ukatili kwa watoto na wanawake kwa lengo la kuiweka jamii salama.

Kanali Abbas ameyasema hayo Machi 08, 2023 kwenye viwanja vya shule ya msingi Amani wilayani Tandahimba katika kilele cha maadhimisho siku ya mwanamke duniani kimkoa ambapo ameeleza kuwa serikali na mkoa unachukua hatua za kukabiliana na vitendo vya ukatili lakini wadau mbalimbali wanahitaji kupaza sauti zao kutokanana na changamoto iliyopo.

Mkuu wa mkoa huyo amesema  serikali itaendelea kushirikiana na wadau na mashirika mbalimbali katika kutekeleza sheria na makubaliano ya kikanda na kimataifa ya kupinga vita vya ukatili wa kijinsia wa mtoto na mwanamke lakini mkoa unakabiliwa na tatizo la mimba za utotoni na waasirika zaidi ni mabinti walio chini ya miaka 19.

Aidha Kanali Abbas amewata wananchi mkoani Mtwara kuwa na dhamira ya dhati ya kumaliza vitendo vya ukatili kwa familia kuacha kukaa kimya yanapojitokeza matendo hayo pamoja na kuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano wa ushaidi wa matukio yanayojitokeza.

Kwa upande wake Mbunge wa viti maalum mkoani Mtwara Mhe. Agnes Hokororo  amewataka wanawake mkoani humo kumuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa ndiye mdau namba moja wa usawa wa kijinsia na ndio maana katika serikali yake wanawake amewapa nafasi katika kila idara.

Aidha amewasisitiza wanawake kujikita katika kuinua elimu kwa kuwa mkoa mkoa umekua na muamko mdogo katika elimu na wanaoweza kufanikisha hilo ni wanawake ambao wanashiriki moja kwa moja kwenye mipango ya kuinua elimu.

Nae Jaji wa Mahakama Kuuu kanda ya Kusini Mhe. Rose Ibrahimu  amewataka Wanawake wajikite katika kusimamia uchumi wa familia na Taifa kwa kutumia teknolojia sambamba na kutumia teknolojia hiyo katika kutambua haki zao za msingi.

Mwenyekiti  wa Mtandao wa Polisi Wanawake mkoani Mtwara( TPF-NET) kutoka dawati la jinsia Mkaguzi  Msaidizi Bahari Sendela amesema mtandao ulianzishwa mwaka 2007 kwa lengo la kuondoa na kuzuia ukatili na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawanke na wanaume hivyo jamii inapaswa kulitumia dawati hili ipasavyo.

Hata hivyo Sendela ameeleza kuwa vitendo vya ukatili inaendelea kumeshamiri kutokana na ushirikianao hafifu uliopo kati ya Wananchi na vyombo vya dola na kupelekea wananchi kutokua ana imani hasa na jeshi la polisi lakini jeshi peke yake aliwezi bali kwa kuunganisha nguvu ya pamoja itawezekana.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa