• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Kamati ya fedha yataka wananchi kujilinda njaa kutokana na uhaba wa mvua na mafuriko

Posted on: March 23rd, 2023

Wananchi wa Halmshauri ya Mji Newala wamepewa angalizo la kujikinga na baa la njaa kufuatia uhaba wa mvua uliojitokeza mwaka huu pamoja na mafuriko yaliyowapata wananchi wanaofanya shughuli za kilimo kwenye ukanda wa bonde la mto Ruvuma.

Rai hiyo imetolewa na wajumbe wa kamati ya fedha kwenye kikao chao kilichoketi Machi 20, 2023 ambapo Mwenyeketi wa Halamshauri ya Mji Newala Mhe. Yusuph Kateule kamewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kuweka akiba ya chakula na kulima mazao yanayostahimili ukame.

“Kwanza sisi tunawapa pole wananchi waliopatwa na janga la mafuriko, Mungu azidi kuwatia nguvu na kuwaweka salama lakini kutokana na hali ya uchache wa mvua kwa mwaka huu na haya mafuriko yalitokea niwaombe wananchi tutunze chakula tulichonacho na kipindi hiki cha mvua kilichobaki tupande mazao yanayoweza kutunusuru au kupunguza makali njaa hali itakuwa mbaya zaidi” 

Aidha Mhe. Kateule amewataka viongozi wa vijiji na kata watoa elimu kwa wananchi juu ya utunzaji chakula na kuanzisha utaratibu mpya wa kuuza mazao yao kwa kutumia vibali visivyo na malipo ili kuzuia uuzaji holela wa mazao pamoja na kudhibiti wizi ulioweza kujitokeza.

Naye Mheshimiwa Hamisi Namata diwani wa Kata ya Mtonya ameeleza kuwa hali ya chakula  kwa wakazi wa Newala kwa sasa sio nzuri hivyo ameimba idara ya kilimo na taasisi zinazousika na utoaji wa taarifa ya hali ya chakula kuieleza serikali kuwa wananchi wa Newala wanahitaji  msaada wa haraka wa chakula kwa kuwa mashambani hakuna mazao ya kutosha na sokoni bei zinapanda kwa kasi.

“Juzi sokoni kiloba cha unga cha kilo 25 kilikua shilingi elfu arobaini jana kilifika mpaka elfu hamsini na leo mpaka muda huu tunaoongea nimepita sokoni nimekuta ni shilingi elfu hamsini tatu na maduka yanayouza unga ni machache kwa kweli hali hii ni mbaya watu wanahitaji msaada” alisisita diwani Namata.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi ambae pia ni Afisa Kilimo wa Halmashauri hiyo Ndg. Calistus Komba amesema hatua za utoaji taarifa kupitia kitengo cha maafa zimeshachukuliwa na sasa wanakamilisha tathmini ili kufikisha mchanganuo wa mahitaji  ili ufikishwe ofisi ya waziri mkuu ambayo ndiyo yenye dhamana na utatuzi wa majanga nchini.

Hata hivyo Komba amewashauri wakulima kutumia mbegu za muda mfupi na kupanda mazao yanayostahimili ukame ili kuendana na hali ya hewa ya mvua chache, ambapo maafisa ugani ngazi kata wapo tayari kutoa ushirikiano wa elimu kwa wakulima kuendana na hali halisi ya hewa hivyo popote kwenye changamoto wasisite kuwatumia kwa ajili ya kupata ushauri.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa