Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

KAMATI YA MFUKO WA JIMBO YA HALMASHAURI YA MJI NEWALA YAIDHINISHA ZAIDI YA TSH. MILIONI 33 KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI

Posted on: November 27th, 2018

Kamati ya Mfuko wa Jimbo ya hamashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara, jana Novemba 26, 2018 imefanya kikao cha kupokea na kuchambua maombi ya miradi ya jamiipamoja ana kuidhinisha Shilingi 33,600,000/= itakayotumika kwenye miradi hiyo.

Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa wialaya chini ya mwenyekiti wake Mbunge wa jimbo la Newala mjini ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa umma na Utawala bora Mhe. George Mkuchika, ambapo kikao hicho kiliamua kupeleka fedha hizo kwenye miradi inayogusa wananchi moja kwa moka kama ilivyo kipaumbele cha serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kamati inapenda kuutarifu umma kuwa Mgawanyo wa matumizi ya fedha hizo umegusa Tarafa zote mbili za halmashauri hiyo na mairadi iliyoidhinishwa ni miradi ya ujenzi na ununuzi wa baiskeli za walemavu, ambapo kwenye mradi wa ujenzi Tarafa ya Mkunya imeidhinishiwa fedha Tsh. 14,000,000/=.

Kati ya fedha hizo Tsh. 4,000,000/= zimeelekezwa kwenye umaliziaji wa nyumba ya waalimu shule ya sekondari Malocho,  Tsh. 1,200,000/= kukamilisha matundu ya sita (6) ya vyoo shule ya msingi Kiuta, Tsh. 2,000,000/= ujenzi wa matundu ya vyoo shule ya msingi Mpilipili, Tsh. 3,000,000/= ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Amani, na Tsh. 3,800,000/= zimeidhinishwa kwenda kutekeleza ujenzi wa nyumba ya waalimu shule ya msingi Matokeo.

Tarafa ya Newala imeidhinishiwa Tsh. 13,600,000/= kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo ya ujenzi, ambapo Tsh. 2,000,000/= zitatumika kujenga kisima shule ya sekondari George Mkuchika, Tsh. 4,100,000/= kwa ajili ya kujenga darasa katika shule ya msingi Kilidu, Tsh. 2,000,000/= kwa ajili ya kumalizia ofisi ya kijiji cha Mahumbika, Tsh. 2,000,000/= kumalizia ujenzi wa Zahanati ya Moneka, Tsh. 1,500,000/= ujenzi wa matundu ya vyoo shule ya msingi Makote, na Tsh. 2,000,000/= kwa ajili ya kumalizia Ofisi ya Mtaa Majengo.

Kamati pia imeidhinisha Tsh. 6,000,000/= kwa ajili ya ununuzi wa baiskeli 10 za walemavu ambao wanne kati yao ni wanafunzi na kamati imeamua kuwapa kipaumbele ili kuendana na sera ya Taifa ya elimu sawa kwa wote sambamba na sera ya elimu bure.

Wanafunzi hao wanaotarajia kupata baiskeli hizo ni Sharibu Hassan wa shule ya msingi Julia, Samko Muksini wa shule ya msingi Tupendane, Zuhura Mohamedi wa shule ya msingi  mkoma 1 na Savia Andrew wa shule ya msingi Nambunga. Wengine ni Jamilu Manzi, Omary Selemani, Ziada Twalibu, Siamini Dadi, Zaituni Ismaili na Udhaifu Issa, huku ndugu Hamisi  Mussa wa kijiji cha Mnanje akitarajia kupokea baiskeli yake kutokana na makubaliano ya kikao kilichopita cha kamati hiyo.

Aidha kamati imewataka watu wote wanaohusika na kuratibu fedha hizo, kuhakikisha akaunti zao za benki zinafanyakazi huku ikitaadharisha juu ya matumizi mabaya na kuahidi kuitembelea miradi hiyo ili kujiridhisha kwenye hatua za utekelezaji wake.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa