• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UTAMBUZI WA WANYAMA

Posted on: August 16th, 2025

Ili kuwa na ufanisi wa zoezi la utambuzi na chanjo ya Ng’ombe, Mbuzi na Kondoo, maafisa mifugo wa halamshauri ya Mji Newala wametakiwa kwenda kuwa elimisha wafugaji juu ya umuhimu wa zoezi hilo pamoja na ruzuku inayotolewa na serikali.

“Chanjo hii ya sasa ni lazima wachangie serikali imetoa ruzuku ya asilimia hamsini na mkulima atatoa asilimia hamsini kwa kila mfugo, napokea simu nyingi wakidai chanjo ni bure sio hivyo nendeni mkawaelimishe wajue”.

Rai hiyo imetolewa na afisa kilimo, mifugo na uvuvi wa halmashauri hiyo Ndg. Calistus Komba wakati anafungua mafunzo ya Mfumo wa Kitaifa wa Utambuzi na Afya ya Mifugo (UTAMBUZI) kwa maafisa hao.

Aidha Komba ameishukuru serikali kwa kuwajali wakulima na kufafanua kuwa mfugaji atachangia shilingi 500 kwa Ng’ombe mmoja na shilingi 300 kwa Mbuzi na Kondoo na kuwahimiza maafisa hao kwenda kufanya kazi yao kwa weledi ili kufanikisha lengo la serikali.

Kwa upande wake Daktari wa mifugo wa halmashauri hiyo Selestine Mgando amesema zoezi hilo ni la kitaifa ambapo kutakuwa utambuzi na kutoa chanjo kwa Ng’ombe kwa ajili ya kuzuia homa ya mapafu na chanjo ya Sotoka ya Mbuzi na Kondoo.

Dkt. Mgando ameeleza faida ya zoezi hilo “kuna faida kubwa sana kwa taifa na wafugaji wenyewe kwanza kabisa tunawakinga wanyama wetu, kudhibiti vifo vya wanyama, kudhibiti wizi na kuwezesha nchi kuingia katika masoko ya kimataifa kwa kukidhi vigezo”.

Hata hivyo Mgando amewasisitiza maafisa ugani kuzingatia mafunzo hayo na kuwaomba wafugaji kujitokeza kuchanja mifugo yao wapate faida mbalimbali ikiwa pamoja na kuongeza uzalishaji wenye tija utakaopelekea kuongeza kipato chao.

Akiwaelekeza washiriki wa mafunzo hayo afisa TEHAMA wa halmashauri Daud Matandiko serikali imeandaa programu maalum ya simu ya kukusanyia taarifa kupitia simu janja kwa ajili ya kufanikisha zoezi la utambuzi

“Na application hii inafanyakazi kwenye adroid peke yake, ni ka application nyepesi itakayo kuwezesha chukua taarifa za mkulima au mfugaji na taarifa za wanyama wake”. Amefafanua Matandiko

Hata hivyo katika zoezi hilo sambamba serikali kutoa ruzuku na chanjo lakini inatoa pete za utambuzi kwa Wanyama, malipo ya uendeshaji zoezi kwa wataalam pamoja na vishikwambi kwa kila afisa mifugo wa kata.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MHE. KUNDYA AWAAGIZA WATAALAM WA KILIMO NA FEDHA KUWAELISHA WAKULIMA KUHUSU UTUNZAJI WA FEDHA

    August 20, 2025
  • TAASISI NA VITENGO VINAVYOSIMAMIA USAFI MSHIRIKIANE KUTOA ELIMU KWA JAMII

    August 19, 2025
  • MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UTAMBUZI WA WANYAMA

    August 16, 2025
  • JAMII YATAKIWA KUWAAMINI VIJANA NA KUWAPATIA FURSA

    August 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa