• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi Newala Mji ahimiza ushirikiano Watendaji Kata, Watumishi Idara ya Afya na Tehama

Posted on: September 16th, 2019

Mkurugenzi wa halmashauri ya mji Newala ndg. Andrew Mgaya, amewataka wakuu wa vituo vya Afya, waratibu wa mfuko wa afya ya jamii uliboreshwa (ICHF) na Chanjo ya Surua-Rubella, kushirikiana na maofisa watendaji wa kata na maafisa Tehama, kuboresha huduma zao ili kufikia lengo kusudiwa la Serikali.

Mkurugenzi Mgaya ameyaeleza hayo leo Jumatatu 16/09/2019, alipokutana na wataalamu hao kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri, cha kujadili mbinu na kupeana uzoefu wa kuboresha utoaji huduma bora kwa wananchi na kufanikisha malengo tarajiwa.

Amesema ili kazi yoyoye ilete mafanikio hakuna budi kuwe na mshikamano wa pamoja na kwenye ngazi ya halmashauri watendaji wa kata ndio wenyenguvu wa kuratibu shughuli zote hivyo uzajili wa CHF iliyoboreshwa na chanjo ya Surua-Rubella ni lazima wawe kwenye nafasi ya uratibu wa zoezi hilo.

“Maagizo haya ni ya serikali na ni yakitaifa hivyo ni lazima tuyatekeleze hakuna namna, hawa watendaji ndio mabosi wenu huko unakofanya kazi, sasa kuanzia sasa ni lazima wawe sehemu ya utekelezaji hasa kwenye ICHF, na ninataka kuanzia leo liundwe group la whatsapp na wao wakiwemo, na wote niliowaita hapa mtatao mrejesho wa kile mnachokifanya kila siku, ili tuone mmefanikiwa wapi na mmekwana wapi ili tushauriane na kupeana uzoefu.” amesisitiza Mgaya.


Hata hivyo Mkurugenzi Mgaya amewataka wataalamu hao kutambua kuwa mfanikio yanatokana na ubunifu wa kiutendaji na hakuna njia yamkato, hivyo huu niwakati wakutumia maarifa waliyonayo kufanikisha mipango ya serikali wanayoitumikia na wananchi ambao ndio walengwa wakuu.

Aidha amewataka wakuu wa vituo vya afya kuzingatia maadili ya kazi, kutunza kumbukumbu zote za mapato na matumizi ya fedha pamoja na dawa, kwani hoja yoyote itakayoibuka muhusika atalazimika kuijibia mwenyewe huku akiwasisitiza kufunga mifumo ya kukusanya fedha (GOT-HOMIS) kwenye vituo vyao kama serikali ilivyoelekeza.

Kwa upande wake mratibu wa CHF iliyoboreshwa wa halmashauri hiyo Bi. Grace Mtulo amesema kutokana na kikao cha leo, anayomatumani makubwa ya kuongeza kasi ya usajili ya kaya kwa kuwa timu imeongezeka, na kwa wale wataoonekana kuwa wazito kwenye zoezi hilo watawekwa pembeni hivyo ameomba uwepo wa ushirikino baina yao.

Naye mratibu wa chanjo halmashauri ya Mji Newala Bi. Marium Shabani, amesema sasahivi wapo kwenye kampeni ya kitaifa yakutoa chajo ya Surua-Rubella inawahusu watoto kuanzia miezi 9 hadi miaka 4 na miezi 11 na chanjo ya polio kwa watoto wa mwaka 1.5 hadi miaka 3.5 zoezi litakaloanza tarehe 26/09/2019 mpaka tarehe 30/09/2019.

Bi. Marium ameitaka jamii kuhamasishana na kujitokeza kupata chanjo hizo, na leongo ni kuwafikia ambao hawajapata kabisa na wale ambao hawajapata kikamilifu kwani kitaifa inaonyesha mpaka sasa waliopata ni 85% huku lengo likiwa ni 100%, na kuongeza kuwa magonjwa hayo hayana tiba, tiba yake ni kinga ambazo ni hizo chanjo.





Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa