• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi Nnauye amewapongeza wataam wa afya na watendaji wa kata utekelezaji mkataba wa lishe

Posted on: July 30th, 2025

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Newala Ndg. Geofrey Nnauye amewapongeza wataalam wa afya na lishe pamoja na watendaji wa kata kwa utekelezaji nzuri wa afua za lishe na kuwataka kugeukia masuala ya usafi.

Mkurugenzi Nnauye ameyasema hayo katika kikao cha robo ya nne 2024/2025 cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ngazi kata, ambapo ameeleza kuwa tathmini kuhusu lishe kata zote vimefikia vigezo na kufanya vizuri.

“Kama tulivyotoka huku kwenye score card ya lishe yote ikawa ya kijani, tumeanza mwaka mpya wa fedha hii julai, jukumu letu la usafi Pamoja na vyoo bora yanaanza lakini sasa tusibweteke ili tusirudi nyuma kwenyemambo yote” Amesisitiza Mkurugenzi

Katika hatua nyingine katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu amewataka wajumbe wa kikao hicho kuwa chachu ya uwepo wa amani na utulivu katika maeno yao kwa kuripoti viashiria vya uvunjifu wa amani.

Kwa upande wake kaimu katibu tawala wa wilaya ya Newala Bi. Mary Twamgabo amefurahishwa na hali ya lishe huku akisititiza elimu ya usafi wa mazingira kwa wananchi iwe ya kudumu kwa kutumia mbinu mbalimbali mpaka jamii ipate uelewa.

“Kuhusu vyoo bora hilo lisiwe sehemu ya kutukatishe tamaa, sisi tuendelee kuwaelimisha na tusisubiri wakati wa mikutano moja moja, kupitia nyumba kwa nyumba, kupitia watoa huduma ngazi ya jamii mwisho wa siku naamini tutafanya vizuri”. Ameeeleza Twamgabo

Afisa afya mazingira wa halmashauri hiyo Ndg. Jackson Lumeya amefafanua hali ya usafi inazidi kuimarika baada ya kuanza kutekeleza kampeni ya kuboresha hali ya usafi wa mazingira Pamoja na ujenzi wa vyoo bora katika robo ya tatu 2024/2025mbapo

Ndg. Lumeya amesema “Tunachoomba ni ushirikiano kwa wananchi na watendaji ili tuweze kufikia malengo ya serikali ya hali ya usafi na tuweze kufikia 100%”

Hata hivyo Lumeya amebainisha kuwa kwasasa hali ujenzi wa vyoo imefikia 59% toka 38% iliyokuwepo wakati wanaanza utekelezaji na kaya zenye usafi wa mazingira 47% toka asilimia 26 ya awali.

Kutokana na taarifa ya hali ya usafi kupitia kikao cha afya ya msingi kubaini kutokuwa na hali ya kuridhisha ya usafi kilifanya uamuzi wa kupata taarifa ya hali ya usafi kwenye kaya na ujenzi wa vyoo bora ya kila robo kupitia kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe ngazi ya kata.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Fedha za mfuko wa elimu shilingi milioni 155 zatekeleza miradi ya elimu Newala Mji

    July 31, 2025
  • WALIMU KIDATO CHA SITA WAPONGEZWA KWA MATOKEO MAZURI

    July 30, 2025
  • Mkurugenzi Nnauye amewapongeza wataam wa afya na watendaji wa kata utekelezaji mkataba wa lishe

    July 30, 2025
  • WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    July 02, 2025
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa