• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi wa halamshauri ya mji Newala, leo Ijumaa Mei 24, 2019 amezindua rasmi zoezi la uandikishaji wanachama wa Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) iliyoboreshwa

Posted on: May 24th, 2019

Mkurugenzi wa halamshauri ya mji Newala, ndugu Andrew Mgaya leo Ijumaa Mei 24, 2019 amezindua rasmi zoezi la uandikishaji wanachama wa Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) iliyoboreshwa kwa kukabidhi simu na vifaa vingine kwa maafisa waandikishaji 59 wa mitaa na vijiji wa halmashauri.

Mkurugenzi Mgaya amekabidhi vifaa hivyo kwenye ukumbi wa mikutano wa hospatali ya wilaya Newala, ambapo amewakata maafisa hao kwenda kufanya kazi kwa bidii kwa kutembelea na kuzihamasisha kaya, vikundi vya jamii na taasisi mbalimbali ikiwemo shule ili wajiandikishe na kuifikia adhma ya serikali ya kuwafikishia wananchi huduma bora za afya kupitia CHF iliyoboresha.

Aidha katika kutoa motisha kwa maafisa hao amewaahidi kutoa shilingi laki moja (Tsh. 100,000/=) kwa afisa atakaefakiniwa kusajili kaya nyingi, kwa kufikisha zaidi ya asilimia 80 ya usajili kwenye maeneo yao na kuwataka kulichukulia jambo hilo kuwa ni fursa kwao.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo amewasihi maafisa hao kuwa waadilifu kaika utendaji kazi wao na ameshauri fedha wanazokusanya ni vema wapeleka kwenye akaunti za bank kila wanapofanya usajili kwani hiyo itasaidia kuondokana na tamaa ya matumizi mabaya ya fedha hizo.

Katika hatua nyingine amewata wananchi wawatambue maafisa hao na kuwapa ushirikiano ikiwa pamoja na kujiunga kwa wingi kwani CHF iliyoboreshwa ndiyo suluhisho la matibabu hasa kwa wananchi wa kipato cha kawaida na ni muhimu kwao kujiunga.


Kwa upande wake Mratibu wa Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) iliyoboreshwa wa halmshauri hiyo Bi. Grace Mtulo amewataka maafisa hao kuwa mfano kwa jamii kwa wao wenyewe kuanza kujisajili kwenye mfuko huo na kufanya uhamasishaji kwa wananchi wengine.

Aidha Bi. Mtulo amefafanua kuwa zoezi hilo ni fursa ya kujiongezea kipato kwa maafisa waandikishaji, kwani ukisajili kaya moja wenye watu 6 gharama yake ni shilingi elfu thelethini (30,000/=)  na asilimia kumi (10%) itarejeshwa kwa muandikishaji.

Sambamba na hilo amevitaja vifaa walivyokabidhiwa kuwa ni Simu 59, vitambulisho, Pochi za kuwekea vitambulisho pamoja na fomu za usajili wananchama huku akiwataka maafisa hao watumie vifaa hivyo kama ilivyokusudiwa na sio kwa mambo yao binafsi.

Hata hivyo Mtulo ameeleza kuwa zipo faida nyingi za kujiunga na CHF iliyoboreshwa, na baadhi ni kaya iliyoandikishwa wenye watu 6 kutibiwa mwaka mmoja bure, kupata huduma kwenye kituo chochote cha afya cha serikali ndani ya mkoa, huduma ya kulaza wagonjwa, upimaji, upasuaji mdogo na ongezeko la dawa.



Wakizungumza kwa niaba ya maafisa wengine waandikishaji Bwana Awadhi Uleme kutoka Mnalale, Bi. Salama Hashimu wa Mkoma 1 na Abdulatifu Halifa kutoka mtaa wa Juhudi-Makonga wamesema wapo tayari kwenda kutekeleza jukumu hilo kwa kuwa mafunzo ya kutekeleza kazi hiyo walishayapata mapema tangu mwezi februari mwaka huu na hatua hiyo itaenda kuwarahisihia kazi.








Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa