• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Newala, aainisha mipango mipya ya vyanzo vya mapato

Posted on: December 7th, 2018


Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Newala mkoani Mtwara Andrew Mgaya, amesema halmashauri yake imeweka mikakati ya kuongeza mapato yake ya ndani kwa kuanzisha vyanzo vipya ya ukusanyaji.

Hayo ameyaeleza jana, Alhamis december 06, 2018 kwenye kikao cha Ushauri wa Maendeleo wilaya ya Newala (DCC), kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya Newala.

Mgaya amesema halmashauri yake imeshachukua hatua za kukabiliana na ufinyu wa mapato na kuacha kutegemea mapato ya serikali kuu na ushuru wa zao la korosho pekee, na kuongeza kuwa baadhi ya vyanzo hivyo  tayari vimeshaanza kuonyesha mafanikio.

Amevitaja vyanzo hivyo kuwa ni pamoja na upimaji shirikishi wa viwanja zaidi ya 300, kuongeza mabucha ya nyama hadi kufikia 10 ndani ya soko kuu, kusimamia tozo za usafi wa mazingira, kuanzisha chumba cha kuifadhia mizigo ndani ya soko, kuanzisha eneo la kushusha mizigo (bandari kavu) na ujenzi wa mabanda 100 biashara.

Mgaya amevitaja vyanzo vingine kuwa, ni hivi karibuni kuanza kutumia mashine ya kuchunguza mwili mzima (full blood picture) kwenye hospitali ya halmashauri, kuanza kutumika kwa zahanati nne na kituo kimoja cha afya pamoja na ujenzi wa mabanda ya biashara karibu na eneo la hospitali.

Hata hivyo Mkurugenzi Mgaya, ameahidi kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa wilaya Mhe. Aziza Mangosongo, ambaye amewataka wakugenzi kukaa na wakuu wa idara kujadili na kuibua vyanzo vipya vya mapato pamoja na kuwawekea maafisa watendaji malengo ya ukusanyaji kwa kila mwezi.

Aidha katika hatua nyingine, kutokana na Mamlaka ya Mapato (TRA) wilayani hapa kuotofanya vizuri kwenye kukusanya kodi za majengo na mabango, Mkurugenzi huyo ameishauri taasisi hiyo kukutana na wataalamu wa halmashauri ili kujifunza mbinu walizokuwa wanazitumia kwenye zoezi hilo.

Taarifa ya TRA ya ukusanyaji kodi 2017/2018 imeonyesha mapato yameshuka kwani kwa halmashauri ya Mji Newala walikadiria kukusanya milioni 40 kwenye majengo lakini hawakufikia lengo kwa kukusanya milioni 26,320,000/- pekee, kiwango ambacho ni tofauti na awali kwani halmashauri ilikuwa inakusanya zaidi.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa