• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Mkoa Mtwara amaliza mgogoro wa ardhi sekondari ya Dr. Alex Mtavala Newala Mji

Posted on: September 23rd, 2019

Mkuu wa Mkoa Mtwara Mhe. Gelasius Gaspar Byakanwa amemaliza mgogoro wa ardhi kati ya wananchi waliotoa maeneo yao kujenga shule ya sekondari Dr. Alex Mtavala na halmashauri ya mji Newala, huku akielekeza kuwa hakuna mwananchi atakayelipwa fidia na serikali mkoani Mtwara, kwakutoa kipande cha ardhi yake kuchangia miradi ya maendeleo iliyoibuliwa na wananchi wenyewe.

Mhe. Byakanwa ameyazungumza hayo mwishoni mwa wiki iliyopita siku Ijumaa 20/09/2019 akiwa katika ziara yake wilayani Newala ya kutatua migogoro ya ardhi, wakati anaongea na pande hizo mbili, ambapo wananchi hao kupitia mwenyekiti wao Said Ibrahim Uledi na katibu wa malalamiko Lezle Chikolo, walikuwa wanailalamikia halmashauri hiyo kutowalipa fidia ya maeneo yao.

Amesema kumekua na tabia mbaya imeanza kujitokeza miongoni mwa wananchi ambao walitoa ardhi yao kwa ajili ya shughuli za maendeleo na baadae wanapoona ukuaji wa miji na  maeneo hayo waanza kuibua migogoro ya kudai fidia kwa tama ya fedha, na hata eneo hilo liliibuliwa kwenye ngazi ya kata hivyo kama ni malipo wangekubailiana kwenye vikao vya awali ngazi ya kata au kijiji na malipo yafanyike huko na huo sio mgogoro, shule hiyo na maeneo yake ni mali ya serikali.

Hata hivyo Mkuu wa mkoa amesema inashangaza kuona viongozi wa walalamikaji, walikua viongozi wakati wa mchato wa kuanzisha shule hiyo, ndg. Said Uledi alikua mweyekiti wa kijiji na Lezle Chikolo alikua Mratibu Elimu Kata wa kata hiyo na wenyewe wanakiri kushiriki na kuhamashisha ujenzi wa shule hiyo na sasa wanageuka kama walikua hawajua kitu chochote.

Aidha amewaomba wananchi kuendelea kujitolea ardhi yao kwa ajili ya kuwezesha maendeleo katika maeneo yao, kwani serikali inandelea kutekeleza miradi iliyoanzishwa na wananchi kama zahanati, shule na miradi mingine lakini makubaliano yote yafanyike kwenye ngazi inayofanyika uibuaji wa miradi hiyo na sio kungoja mradi umeshatekelezwa ndio unaanza kuibua sintofahamu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri hiyo ndg. Andrew Mgaya, amekiri kufikiwa na malalamiko ya wananchi hao, lakini amesema aliwajibu kwa maandishi kuwa suala hilo wakalimalize kwenye ngazi ya kata, kwani wao wenyewe ndio waliuanzisha mradi huo na serikali kupitia halmashauri waliukamilisha kama muongozo wa mwaka 2005  wa utekelezaji wa miradi ya maendele unavyoelekeza.

Naye mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mhe. Sambili Mohamedi, amesema wananchi hao sio wa kweli kwa kuwa tangu shule hiyo inaanzishwa mwaka 2006 na shule zingine zote za kata zilizoanzishwa wakati huo wilayani Newala, hazikuwa na migogoro yoyote zaidi ya mgogoro mmoja katika kata ya Mcholi 1, vijiji vikigombania shule hiyo ijengwe kwenye kijiji chake lakini wananchi waliridhia kutoa maeneo yao.

Shule ya sekondari ya Dr. Alex Mtavala ipo mtaa wa Legeza kata ya Julia halmashauri ya Mji Newala, mchakato wa kuanzishwa kwake ulianza mwaka 2006 eneo hilo likiwa kata ya Luchingu na kusajiliwa rasmi mwaka 2008.



Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Serikali imesema wanawake na vijana wanaweza kukuza kilimo biashara na kuwa endelevu

    August 01, 2023
  • Mkuu wa mkoa Mtwara aridhishwa na utekelezaji wa miradi ya BOOST na ujenzi wa mabweni

    July 29, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa