• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Newala Town Council
Newala Town Council

Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • TEHAMA na Mahusiano ya Umma
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya
      • Maji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi, Maliasili na Mipango Miji
      • Kazi
      • Usafi na Mazingira
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Maji
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Habari
    • Matukio
    • Video
    • Maktaba ya picha

Mkuu wa Wilaya ya Newala December 29,2018, Amezindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali wadogo

Posted on: December 31st, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo Jumamosi December 29,2018, amezindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wilayani hapa, huku akitoa onyo kwa watakao toa taarifa za uongo kuwa watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa pamoja na kunyang’anywa kitambulisho.

Akizindua zoezi hilo, lililoitikiwa na wajasiriamali zaidi ya 1000 na 594 kati yao kupata vitambulisho hivyo wakati wa uzinduzi, Mhe. Mangosongo  amesema wanaostahili kupata  vitambulisho hivyo ni wale wenye sifa tu huku akimshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwaona wananchi wa hali ya chini walioamua kujitafutia kipato chao kwa njia halali, na kuamua kuwapunguzia adha ya tozo za ushuru kutoka kwa taasisi mbalimbali za fedha walizokuwa wanazilalamikia kwa muda mrefu.

Afisa wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilayani Newala, bwana Yusuph Otieno, amesema wanaostahili kupata vitambulisho hivyo vilivyotolewa na Mhe. Rais ni wale wasio na namba ya utambulisho ya mlipa kodi ya biashara (TIN) na mauzo ghafi ya biashara zao yasiyozidi shilingi milioni 4 kwa mwaka au mauzo ya wastani wa shilingi  elfu 12 kwa siku.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kuchukua vitambulisho hivyo, wamemshukuru Mhe. Rais kwa kuwajali na kuwathamini kwani awali walikuwa wanasumbuliwa sana na Maafisa kutoka idara za fedha za halmashauri, TRA na wakati mwingine Mgambo wanaotumwa kukusanya mapato ambao walikua hawaangalii hali ya kipato chao.

Aidha wamemuomba kuendelea kuwaangalia wananchi wa hali ya chini, huku wakiahidi kumuunga mkono kwenye jitihada zake za kuwatumikia watanzania katika kuwaletea maendeleo, uzinduzi huo umefanyila kwenye maeneo mawili tofauti wilayani hapa, ukumbi wa halmashauri ya wilaya Newala na Ofisi ya kata Kitangari.

Rais Dkt. Magufuli hivi karibuni alitangaza kuwapatia vitambulisho vyenye namba ya utambulisho  wajasiriamali wote wadogo nchini, wenye mtaji wa mauzo ya biashara zao yasiyozidi milioni 4 kwa mwaka ambapo mjasiriamali huyo atatakiwa kulipia shilingi elfu 20 kwa mwaka mmoja.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI YA AJIRA MTENDAJI WA KIJIJI January 25, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILI MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III April 14, 2023
  • WITO WA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA January 21, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KUWA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA BVR OPERATORS JIMBO LA NEWALA MJINI January 14, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WANAUME WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI MASUALA YA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    July 02, 2025
  • HOSPITALI YA WILAYA YA NEWALA IMEANZA KUTOA MATIBABU YA VIUNGO KWA NJIA YA MAZOEZI

    July 01, 2025
  • Bilioni 21.5 baji ya Mji Newala 2023/2024

    August 04, 2023
  • Tupo nanenane kutoa elimu kwa wananchi itakayobadilisha mitazamo yao kwenye kilimo.

    August 02, 2023
  • Tazama zote

Video

Video nyingine

Kurasa za Haraka

  • Sanitation day
  • Tender
  • Uhuru torch

Kurasa Mashuhuri

  • Higher Education Students' Loans Board
  • National Examinations Council of Tanzania
  • Tanzania National Electoral Commission
  • PSPF Pension Fund
  • Public Service Management
  • President's Office Regional Administration and Local Government

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Newala-Mtwara

    Anwani ya Posta: P.O.BOX 39

    Simu: (+255) 023 2935398

    Mobile: PS (0684439199)

    Barua pepe: info@newalatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Disclaimer
    • Sera ya Faragha
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya eneo la tukio
    • Huduma

Haki miliki©2017 NTC. Masharti yote yanazingatiwa